Wednesday, January 30, 2013

WAKULIMA WA KOROSHO LINDI NA MTWARA WAPONEA BAKARI KICHWA

Wakulima wa Korosho katika Mikoa ya Lindi na Mtwara wako katika hali mbaya ya kipato, baada ya korosho walizokopesha katika stakabadhi ghalani kuanzia mwezi Octobar mwaka jana hawajalipwa mpaka sasa.

"Bakari kichwa na majani ya mhogo au kisavu ndio mboga tunayokula kila siku kwa kutokana na ukata wa kukosa pesa niliyokopesha korosho toka mwaka jana, fungu la Bakari kichwa linauzwa Tshs. 1000 na Bakari kichwa mmoja anauzwa Tshs. 100, hali ni mbaya hata watoto wameshindwa kwenda shule toka imefunguliwa kwa sababu sina kilo 60 ya mahindi, kilo 40 ya maharage na kilo 40 ya mchele pamoja na ada ya shule Tshs. 20000 kwa mwanafunzi wa sekondari," alisema Lidia Chinguile Mkazi wa Masasi Mtwara.

Waziri wa Kilimo na Chakula Mhandisi Christopher Chiza aliwaahidi wakulima wa korosho tarehe 3 mwezi wa 12 mwaka 2012 alipofika katika Wilaya ya Nachingwea Mkoa wa Lindi akiwa katika ziara na Rais Jakaya Kikwete, alisema wakulima wote wa korosho watalipwa pesa zao walizokopesha korosho ghalani baada ya wiki mbili.

0 comments:

Post a Comment