Monday, January 21, 2013

MAABARA BADO NI TATIZO SUGU KATIKA SHULE ZA SEKONDARI ZA KATA MTWARA

Hicho ndio chumba cha darasa kinachotumika kama maabara katika shule ya sekondari Dr. Alex iliyoko katika Wilaya ya Newala katika Mkoa wa Mtwara, Wilaya hiyo ina shule za sekondari za kata 28 lakini kati ya hizo ni shule nne tuu ambazo zina majengo mbalimbali ya maabara nazo ni Nambunga, Newala day, Nangwanda na Mnyambe.

"Nasoma masomo ya sayansi lakini hakuna maabara ya uhakika ya kujifunza mambo mbalimbali ya kisayansi, kama unavyoona hivyo ndio vifaa vya kujifunzia unaweza kuingia katika darasa hili kwa ajili  kujifunza ukakuta majiko hayana mafuta ya taa ambayo utawesha na kuchemshia baadhi ya madawa, basi tunasoma tuu kwenye vitabu ukifika mtihani wa vitendo unaferi kwa sababu hujui chochote cha kufanya unapata sifuri," alisema John Nandule mwanafunzi wa kidato cha tatu katika shule ya sekondari Dr. Alex

Mkurugenzi wa Wilaya ya Newala Abdallah Chikota alisema kuwa, tatizo la ukosefu wa maabara lipo katika Wilaya yake lakini kwa sasa wameanza ujenzi wa majengo ya maabara katika baadhi ya shule za sekondari, lakini itachukua muda mrefu kumaliza na kuweka vifaa vya kisasa, maana majengo hayo yanatakiwa katika shule 24. Wanafunzi wa masomo ya sayansi wasome kwa shida shida masomo hayo kwa sasa lakini baada ya muda tatizo hilo litakwisha.

0 comments:

Post a Comment