Sunday, January 27, 2013

KUTANA NA ABIRIA WANAONING'INIZA ROHO ZAO BAHARI

Baadhi ya Abiria nilikutana nao kwenye Mtumbwi katikati ya Tanga na Wete nikielekea visiwani Wete Pemba, upakiaji wa abiria kwa kutumia Mtumbwi, Ngalawa, Mashua na Jahazi sio salama kwa wasafiri mbalimbali wanaotumia Bahari, Ziwa na Mto kusafiri.
"Sio kama tunapenda kuning'iniza roho yangu kwa kupanda katika Mtumbwi na mizigo lakini kwa sababu sina pesa Tshs. 16,000 nauli ya kupanda Meli, humu nalipa Tshs. 8000 kutokana na ugumu wa maisha ndio inanilazimu kuhatarisha maisha yangu kiasi hiki ili kubakiza hiyo Tshs. 8000 nikale nyumbani na watoto," alisema Juma Khamis Shoka mkazi wa Wete.
Afisa wa Sumatra Mkoa wa Tanga Bwana Kamata alisema kuwa, ni makosa makubwa kwa mmiliki wa chombo cha aina ya Mtumbwi, Mashua, Jahazi na Ngalawa kusafirisha abiria. Kazi kubwa ya vyombo hivyo ni kusafirisha mizigo mbalimbali na sio abiria, Sumatra wakimkamata nahodha wa chombo anafikishwa Mahakamani na mmiliki wa chombo anafutiwa leseni ya kumiliki chombo hicho.
Kwa sasa Nchini Tanzania huo ndio usafiri wa pekee katika maeneo mengi yenye Bahari, Ziwa na Mto  na ndio vinavyoongoza kwa kuzama na kuuwa abiria.

0 comments:

Post a Comment