Saturday, January 12, 2013

MAANDALIZI YA SHULE YA PAMBA MOTO JIJINI DAR

Baadhi ya Wakazi wa Jijini Dar es salaam, wakinunua vifaa mbalimbali vya shule katika Soko la Mchikichini Wilaya ya Ilala Mkoani Dar, Wakazi hao wamelalamika kupande kwa bei kwa vifaa hivyo, kiatu cheusi cha mtumba kwa mtoto wa darasa la pili kinauzwa kuanzi Tsh. 20,000 hadi Tsh.30,000, Mwaka jana kiatu kama hicho kilikuwa kinauzwa Tshs. 10,000 hadi Tshs.15,000. Wafanyabiashara walio wengi katika soko hilo ni vijana ambao wameacha utumiaji wa madawa ya kulevya na uporaji na kuamua kujiajiri wenyewe.
"Nimeanza biashara ya kuuza viatu vya aina mbalimbali kwa muda wa miaka 3 sasa, biashara ni nzuri napata pesa ya kujikimu na familia yangu, kabla ya kuja hapa sokoni mchikichini nilikuwa mtaani tuu nakabakaba watu huko kwetu Masasi Mtwara, lakini kwa sasa nimeacha ukabaji kwa sababu napata pesa ya kutosha katika biashara ya kuuza viatu, kwa siku napata mpaka Tshs. 80,000 biashara ikiwa nzuri kama biashara mbaya napa Tshs.30,000 kwa siku," alisema Salumu Manzi.

0 comments:

Post a Comment