Saturday, January 19, 2013

UKOSEFU WA MAKTABA KATIKA SHULE ZA SEKONDARI ZA KATA BADO NI TATIZO SUGU MTWARA



Hiki ni moja ya  chumba kinachotumika kama Maktaba ya shule ya Sekondari ya Nangwanda iliyoko katika Wilaya ya Newala Mkoa wa Mtwara, Wilaya hiyo inashule za Sekondari za Kata 28 na jengo moja la  Maktaba  katika shule ya  Sekondari ya  Newala day.
"Tunapata shida sana ya kusoma kwa sababu ya kukosa vitabu vya uhakika hapa shuleni, ukitaka vitabu lazima uwende kusoma au kuazima katika shule ya sekondari ya Newala day ambako ni zaidi ya kilometa 7 kutoka hapa ninaposoma mimi tena unatembea kwa mguu, muda mwengine ukifika unamkuta mwalimu anayetunza fungua ya maktaba hayupo amekwenda bank kufuata mshahara basi inakulazimu kurudi shuleni bila ya mafanikio ya kupata kitabu,"alisema Juma Mussa Mwanafunzi wa kidato cha pili katika shule ya Sekondari Mtangalanga.
Zaidi ya Shule 27 katika Wilaya ya Newala hazina Maktaba za uhakika ambazo zina vitabu vya masomo mbalimbali wanayofundishwa wanafunzi katika shule hizo, vyumba hivyo vya kusomea kama maktaba  kwa sasa viko katika hali mbaya na havilidhishi kwa mwanafunzi kusoma na kuelewa kile alichokikusudia kusoma.
Mkurugenzi wa Wilaya hiyo Abdallah Chikota alisema kuwa, tatizo la ukosefu wa maktaba katika Wilaya yake ni kubwa sana shule ambazo hazina jengo la maktaba ni 27 kwa sasa, kutokana na  hali hiyo inawalazimu kutumia chumba cha darasa kama maktaba ili waweze kusoma lakini hata hivyo vyumba vya madarasa wanavyotumia kama maktaba viko katika hali mbaya.

 Hali halisi ya ufaulu kwa wanafunzi wa shule hizo bado upo chini kutokana na kutokuwa na sehemu rasmi ya kusomea wakati wa usiku, kwa sasa tumeanza ujenzi wa Maabara katika shule za sekondari mbalimbali tukimaliza ujenzi ndio tutaanza ujenzi wa maktaba katika shule hizo. 

0 comments:

Post a Comment