Saturday, January 12, 2013

MTU NI AFYA IKIWA PAMOJA NA KUJISAIDIA SEHEMU SAFI SIO VICHAKANI

Baadhi ya Abiri wa kwenda Mikoa ya Songea, Mbeya, Mwanza na Bukoba wakipata huduma ya choo katika eneo la Mkambalani Wilaya ya Morogoro katika Mkoa wa Morogoro. Huduma hii ya choo ni salama kwa wasafiri mbalimbali kujisaidia wakiwa njiani, kwa sababu kuna maji ambayo watatumia kujisafisha baada ya kujisaidia, pia inawakinga na magonjwa mbalimbali ya kuambukiza kwa abiria kujisaidia katika vichaka ambavyo mabasi husimama kwa pamoja katika eneo moja na abiria hushuka kujisaidia bila hata ya kuwa na maji ya kujisafisha.
Sehemu kubwa ya barabara za kwenda mikoani mbalimbali hapa nchini Tanzania, hakuna huduma ya choo abiria wengi hulazimika kujisaidia katika vichaka mbalimbali, sio tu kuhatarisha afya zao bali ni uchafuzi wa mazingira kwa kujisaidia sehemu ambayo sio rasmi kwa huduma hiyo.

0 comments:

Post a Comment