Thursday, January 10, 2013

MATUMIZI MABAYA YA BAJAJI ZA KIKWETE NACHINGWEA

Mganga Deus Mosha akitokea katika kijiji cha Lihonji Wilaya ya Nachingwea Mkoa wa Lindi, wakiingia katika Hospitali ya Wilaya kuchukua dawa za kupunguza makali ya ugonjwa wa Ukimwi (ARVs), Bajaji hiyo haitumiki kuwabeba  wamama wajawazito mbalimbali katika kijiji hicho kutokana na ubovu wa barabara. "Haijawahi kubeba mama mjamzito toka imeletwa katika zahanati ya Kijiji cha Lihonji kutokana na ubovu wa barabara, kuwa na mashimo mengi ukimpakia mama mjamzito ambaye ameshindwa kujifungua katika zahanati kwa matatizo mbalimbali ya uzazi kama kondo la nyuma la uzazi kutangulia mbele, kifafa cha mimba, presha kuwa juu, kutokwa damu nyingi wakati wa kujifungua na kondo la nyuma la uzazi kugoma kutoka baada ya kujifungua,ukimleta katika hospitali ya Wilayani anaweza jifungulia njiani au kupata madhala mangine makubwa ya uzazi,"alisema Mganga Deus Mosha.

0 comments:

Post a Comment