Wednesday, January 16, 2013

SAMAKI PWEZA SIO TU KUTABILI MECHI ZA MPIRA WA MIGUU AFRIKA NA ULAYA? BALI ANALETA KHESHIMA NDANI YA NDOA


"Licha ya kutabili mechi mbalimbali za mpira wa miguu katika Bara la Afrika na Ulaya lakini, ukitumia supu ya samaki pweza inaludisha kheshima ndani ya ndoa, kwa kunywa supu hiyo na mkia wake iliyopikwa vema kwa dakika 30 na kuwekwa viungo vya kukata shombo kama ndimu na tangawizi, ukinywa hiyo baada ya saa moja mambo safi ndani ya ndoa," alisema Mfaume Namkopi mpika na mkaanga pweza wa sokoni feri kwa miaka 21 sasa.
Victar Mwandike ni Afisa Uvuvi wa Sokoni hapo alisema kuwa samaki jamii ya Kamba, Kitaa na Pweza wanaongeza vitamini A katika mwili wa binadmu na huleta kheshima katika tendo la ndoa, samaki pweza akiwa mkubwa kuanzia kilo 8 hadi 9 na akikaa vema kitika mwamba anaweza kumuuwa mvuvi wa pweza kwa kumtumbukiza mikia yake sita puani, masikioni,mdomoni na machoni, mvuvi akiwa hana vifaa vya kujikinga anapoteza maisha. Pweza anakuwa mkubwa mpaka kufikia kilo 50 hadi 60 akiwa ndani ya maji na anapenda kuishi chini ya mwamba.
Mfaume Namkopi mpikaji na mkaangaji Samaki aina ya Pweza katika Soko la Kimataifa la Samaki Feri Jijini Dar es salaam, kazi ya kutengeneza pweza inamnufaisha yeye na familia yake, kwa siku anachemsha na kukaanga zaidi ya sahani 20, kila sahani analipwa Tshs. 2000. Msingi wake ni Tshs. 100,000 kwa kununua mzigo wa kuni na mafuta ya kukangia pweza, kwa mwezi analipa kodi ya sehemu ya kukaangia pweza ni Tshs. 15,000.Hajawahi kunywa maziwa hata mara moja kwa kazi hiyo ya kukaa jikoni kwa muda mrefu, kwa siku anapata Tshs 10000 hadi Tshs. 20000 pesa inayokizi mahitaji yake.
Kwa sasa kilo moja ya samaki pweza inauzwa Tshs. 6,000 kwa pweza wakubwa na kwa pweza wadogo kilo moja ni Tshs. 4,000.

1 comments:

  1. hii safi bila shaka.. . japo siajaona uzoefu zaid kutoka kwa makabila mengine kama watu wa tanga na zanzibar (wanaoishi mwambao) ili nielewe vema

    ReplyDelete