Monday, January 28, 2013

UKOJOAJI WA BARABARANI ULIVYOKITHIRI TANZANIA

Baadhi ya abiri wa kwenda Mikoa ya Kusini Lindi na Mtwara, wakijisaidia katika kichaka ambacho kipo karibu na barabarani katika Kijiji cha Ikwiriri Wilaya ya Rufiji Mkoa wa Pwani. Aina hii ya kujisaidia sio tuu kuchafua mazingira pia ni hatari kwa afya inachangia magonjwa ya kuambukiza.

Hivi karibuni Waziri wa Uchukuzi Dr. Mwakyembe alisema kuwa, basi litakalo kamatwa linashusha abiria kwenda kujisaidia kichakani watachukuliwa hatua kali. Je? atatumia njia ipi ili kuwakamata abiria na dereva wa basi? Barabara mbalimbali za kwenda Mikoani hapa Nchi hakuna vyoo vya kujisaidia abiria inawalazimu kujisaidia vichakani na kuchafua mazingira, tena madereva wanajua sehemu maalumu za kujisaidia kwenye vicha mbalimbali mpaka imepelekea sehemu hizo kuwa na biashara kwa sababu abiri hujisaidia kwa dakika tano hadi kumi.

0 comments:

Post a Comment