Monday, February 25, 2013

UTAPIAMLO BADO UPO TANZANIA?

Wakati jamii mbalimbali wakifikiri kwamba ugonjwa wa Utapiamlo umeisha lakini katika Jimbo la Mwibara wilaya Bunda mkoa wa Mara katika kata ya Kibara na Kisori ugonjwa huo bado upo.
Sababu kubwa ya kuwa na ugonjwa huo ni ukame kwa kukosa mvua za kutosha pamoja na kupungua kwa samaki na dagaa katika ziwa Victoria na wanaovuliwa wanaishia kwenye viwanda vya samaki kwa kutengeneza minofu na kusafirishwa nchi mbalimbali.

Watoto hao wangekula samaki na dagaa kwa wingi wangeweza kupata madini ya chuma na protini kwa wingi na ingeweza kupunguza ugonjwa huo.
Kati ya watoto 17,570 watoto 294 wanaumwa ugonjwa wa utapiamlo ambayo ni sawa na asilimia 1.5.

0 comments:

Post a Comment