Sunday, February 24, 2013

HUYU NDIO WANAMKE SHUJAA?

Boke Makori ni wifi yake na Nyangeta Maiga Makori wakazi wa kijiji cha Nyambono wilaya ya Musoma vijijini, Boke ndiye 'WANAMKE SHUJAA' aliyemshawishi kaka yake Mwita Makori kuuza ng'ombe ili wapate nauli ya kumpeleka wifi yake kituo cha afya Manyamanyama Bunda ili ajifungue katika uwangalizi wa wataalamu.

"Wifi akiwa na ujauzito wa miezi nane nilianza kumshawishi kaka kuuza japo ng'ombe mmoja ili tupate nauli ya kumpeleka wifi kituo cha afya alikataa kwa mara ya kwanza, lakini sikuchoka kumwambia kila ninapokwenda kumuona wifi maendeleo yake, niliendelea kumwambia zaidi ya mara tano ndio alikubali kipindi hicho Nyangeta alikuwa na ujauzito wa miezi tisa,"alisema Boke

Kwa upande wake mume wake Nyangeta Bwana Mwita Makori alisema ni kweli dada alikuwa akinihiza kuuza ng'ombe mmoja ili apate nauli ya kumpeleka mke wangu kujifungua katika kituo cha afya, nilikubali kwa shingo upande kwa sababu dada amening'ang'aniza kuuza ng'ombe, nilichaguoa kang'ombe kadogo nikauza kwa Tshs. 15,0000.


"Sasa nimeona umuhimu wa kuuza kang'ombe kangu kadogo ili mke wangu apate nauli ya kwenda kituo cha afya, amejifungua vema watoto mapacha ndio nimefika kumchukua kumrudisha nyumbani Musoma vijijini, nawashauri wanaume wa mkoa wa Mara kuwatunza wajawazito na kuwapeleka katika kituo cha afya kujifungua sio kung'ang'ania wakezao kujifungua kwa wakunga wa jadi,"alisema Mwita

Dereva wa Bodaboda Chacha alisema kuwa nasikia fahari kubwa sana kumbeba mama mwenye watoto mapacha kumrudisha kijijini, nitaendesha pikipiki pole pole na kukwepa mashimo ili mama na watoto wafike salama.

Ghalama za kukodi pikipiki kutoka kijijini Nyambono mpaka Bunda ni Tshs. 60,000 kwenda na kurudi kijijini, ni wanawake wangapi wanaowashawishi kaka zao vijijini kuuza ng'ombe, mbuzi,kuku pamoja na mazao ya kilimo ili ipatikane nauli ya kumpeleka mjamzito pindi anapoumwa uchungu kituo cha afya au hospitali?

Ni wanaume wangapi wanaokubali kuuza rasilimali ili mkewe ajifungulie katika kituo cha afya kwa uwangalizi wa wataalamu? kumbe inawezeka kupunguza vifo vya akinamama kwa jamii kubadilika kwa kutoa msaada kwa mjamzito akikalibia kujifungua?

Safari ya kuelekea kijijini ndio hiyooo imeanza kwa familia ya Makori? nadhani atawatunza vema watoto hao mapacha aliowapata ili wawe viongozi  wa baadae katika nchi yetu ya Tanzania.

0 comments:

Post a Comment