Sunday, March 24, 2013

GOFU LA NYANZA CO-OPERATIVE UNION

Gofu la chama cha ushirika cha Nyanza lililopo katika kijiji cha Nassa katika wilaya ya Nyashimo mkoa mpya wa Simiyu. Ndani ya gofu hilo kuna vinu vya kuchambua pamba na kukamua mafuta ya mbegu za pamba, kwa muda mrefu sasa vinu hivyo havitumiki na wakulima wanapeleka pamba kuchambua katika wilaya ya Bunda mkoa wa Mara. Kwa sasa wakulima wa pamba wako katika kilimo, kilo moja ya pamba kwa mwaka jana ilikuwa shilingi 630.

0 comments:

Post a Comment