Wednesday, April 10, 2013

TRANSFOMA LAZUA KIZAAZAA KARIAKOO JIONI YA LEO

Transfoma ya umeme imezua kizaazaa Kariakoo majira ya saa 17:15 jioni katika mtaa wa Kongo na Muhonda baada ya Transfoma hiyo kuripuka moto na kuanza kutoa moshi mzito uliopelekea baadhi ya wafanyabiashara wa maduka katika mtaa huo kufunga maduka yao kwa kuhofia wizi na kuripuka kwa moto mkubwa katika eneo hilo. 

Transfoma hiyo imekuwa ikiripuka moto na kutoa moshi mzito mara kwa mara na kuleta hofu kwa wafanyabiashara wanaofanya biashara katika eneo hilo na wapita njia, Aidha wafanyabiashara katika eneo hilo wanaiomba Tanesco kuwabadilishia Transfoma hiyo ili kuepukana na madhara makubwa ya moto utakaosababishwa na Transfoma hiyo.

0 comments:

Post a Comment