Thursday, April 4, 2013

HATA WANAWAKE WANAWEZA

Fatuma Abasi na Bibi Halima wakazi wa kijiji cha Lukuledi wilaya ya Masasi mkoa wa Mtwara, wakiwa shambani wanapalia zao la mahindi, zao hilo linapaliwa mara tatu katika kipindi cha ukuaji wake, kipindi cha kwanza yakiota, kipindi cha pili kiwa kimo cha kati na kipindi cha mwisho cha kupalia yakiwa yamebeba mahindi. Kwa sasa guni moja la mahindi linauzwa kuanzia shilingi 90,000 hadi shilingi 100,000, Fatuma na Bibi Halima wamelima heka mbili kama kutakuwa na mvua za kutosha wanatarajia kuvuna magunia zaidi ya 50.


Chiku Juma mkazi wa kijiji cha Kiegei katika wilaya ya Nachingwea mkoa wa Lindi, akioneakana anapanda mahindi katika shamba la heka tano, shamba hilo amelima yeye mwenyewe akisaidiwa na kaka yake Musa Juma.



Amina Bakari na Hawa Mtumba wakazi wa kijiji cha Ikwiriri wilaya ya Rufiji mkoa wa Pwani wakibeba gunia la mkaa kupeleka katika basi la kutoka Mtwara, Wanawake hao ni wafanyabiaashara ya kaa kwa muda wa miaka mitano sasa wamekuwa wakifanya kazi hiyo ambayo wanafanya wanaume hapa nchini, gunia moja la mkaa kwa sasa ni shilingi 35,000 hadi shilingi 40,000.
Kwa siku wanauza magunia 10 hadi 15 ya mkaa wa wasafiri mbalimbali wanaotoka katika mikoa ya Lindi na Mtwara.





 Baadhi wa Wanawake niliokutana nao katika Barabara ya Bibi Titi jijini Dar es salaam, Wanawake hao wakiwa wameucha usingizi baada ya kazi ya kuombaomba bila ya wasiwasi huku wakiwa na watoto wadogo, lakini Wanawake hao wamekuwa wakikaa eno hilo kwa kuomba wapita njia mbalimbali ili waweze kupata pesa ya matumiazi ya kila siku. Wanawake kama huwa wenye nguvu na viungo vyao vimekamilika na wana uwezo wa kulima na akajipatia kipato na kuitunza familia yake kijijini! kwa nini wanawake hawa wanaomba na kuwatesa watoto ambao hawana hatia!

0 comments:

Post a Comment