Ukimsikiliza Zaituni Ally (35) anayeishi na virusi vya ukimwi (VVU) kwa miaka saba sasa, machozi yanaweza kukutiririka mashavuni.
“Nakula mlo mmoja kwa siku siku nyingine nalala na njaa,”alisema Zaituni.
Siyo hivyo tu. Zaituni ana watoto watatu wenye umri wa miaka 9, 5 na miezi mitatu. Alimzaa mtoto wake wa kwanza, ambaye hivi sasa yuko Mtwara kwa dada yake, akiwa hana maambukizi lakini alijifungua mtoto wa pili na watatu akiwa ameshagunduliwa kuwa na VVU.
Hivi sasa mtoto wake wa pili naye anatumia dawa za ARV. Amegunduliwa kwamba ana VVU, japokuwa alipozaliwa alikuwa hana.
Zaituni anasema alipewa maelekezo ya namna ya kumtunza mtoto wake kila alipokwenda kliniki.
“Nilifurahi sana kuambiwa mtoto wangu hana maambukizi alipozaliwa. Niliambiwa nimlee vyema ila cha msingi nilitakiwa kumtengea vifaa vyake vya kutumia kama wembe na sindano,” alisema Zaituni
Ni vigumu kujua lini mtoto huyu alipata maambukizi lakini hali yake iligundulika baada ya kufikisha miaka minne. Na japokuwa ni vigumu kujua namna alivyoambukizwa, maisha ya Zaituni yanatoa ushahidi wa aina Fulani. Hana mume kwa sababu baba ya watoto wake wapili wa kwanza alimuacha baada ya kugundua mama na mtoto wana VVU.
“Umasikini wa kipato ndio umechangia kumuambukiza mtoto wangu virusi vya ukimwi,” alisema Zaituni, huku akibubujikwa na machozi shavuni.
Afisa habari kutoka tume ya kudhibiti ukimwi nchini (TACAIDS) Glory Mziray anasema kuwa, tatizo la Zaituni kukosa chakula na watu wengine wenye tatizo kama lake, wanatoapesa katika kila halmashauri zote nchini ili, kuwawezesha kufanya muitikio wa kudhibiti ukimwi kwa kuwashirikisha watu wanaoishi na virusi vya ukimwi.
Mziray alisema kuwa wilaya inatakiwa kupanga na kujua kuna waathirika kiasi gani na kuwapatia mahitaji mbalimbali wanayowahitaji, kwa mfano chakula, mavazi,elimu kwa jamii juu ya kujikinga na virusi vya ukimwi kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto.
“Haki za watu wanaoishi na virusi vya ukimwi na ukimwi vinajumuishwa na kulindwa katika kila sekta, pia kuna mkakati na sera kwa watu wanaoishi na virusi vya ukimwi wa mwaka 2008 hadi 2012, ili kuweza kuratibu watu hao katika kila sekta, maana watu wanaoishi na virusi vya ukimwi wako katika kila sekta hapa nchini, pamoja na kuunda baraza la watu wanaishi na virusi vya ukimwi ili waweze kujadili haki zao na kuzitatua,” alisema Mziray
Mziray alisema kuwa kila mwaka wanatumia Bilioni 15.5 pesa za kuthibiti ukimwei, pia pesa hizo zinapelekewa katika kila halmashauri kulingana na mahitaji hali ya halmashauri husika, lengo kubwa ni kuhakikisha kuwa wanapambana na maambukizi mapya na kuwapatia mahitaji ya muhimu kwa watu wenye virusi vya ukimwi, hata nchi nyingine kama Kenya, Uganda,Rwanda nao wanawapatia pesa halmashauri husika kudhibiti ukimwi kama tunavyofanya hapa nchini.
Katika Kitabu cha pili cha mkakati wa taifa wa kudhibiti ukimwi cha mwaka 2008 hadi 2012 kinaeleza kuwa, kuhakikisha uwianishaji kwa ukamilif wa changamoto zinazohusu janga la ukimwi katika sera na mipango mikuu ya maendeleo ya muda mrefu, kwa kuzingatia athari mahususi kwa watu wanaishi na virusi vya ukimwi na ukimwi, familia zao zilizoathirika pamoja na masuala yanayohusu jinsia na umasikini.
“Ningekuwa na pesa ya kununua wembe, sindano, chanuo na sabuni mtoto wangu asingepata maambukizi. Lakini hata pesa ya kununua unga na mboga ni tatizo kwangu; nitawezaje kupata pesa ya kununua vifaa mmbalimbali vya kutumia mtoto pekee yake? Kikubwa ninachoangalia ni watoto kupata chakula.”
Akikosa kabisa chakula, Zaituni analazimika kutumia dawa zake za ARVs hivyo hivyo na kumuombea mtoto wake chakula kwa majirani ili asiregee na dawa anazotumia.
Mtoto wa pili wa Zaituni hajui kwa nini anapewa dawa kila siku. Anasema mama yake anampatia dawa asubuhi na jioni; muda mwengine akisahau, inabidi amkumbushe
Mtoto huyo alisema kuwa mama yake alimwambia akinywa dawa hiyo ndio anakua haraka. Pia, aliongeza kwa kusema kuwa anaamini akifikia umri wa kuanza shule akuwa na akili nyingi shuleni kutokana na dawa hizo.
Maamuzi ya kumpeleka wake wa kwanza kwa dada yake yalimsaidia mtoto huyo kutopata maambukizi ya virusi vya ukimwi, mwaka 2006 alianza kliniki na kupimwa akakutwa na maambukizi ya virusi vya ukimwi. Kwa wakati huu, Zaituni bado hajui kama mtoto wake watatu ana maambukizi ya VVU; amemleta katika hospitali ya wilaya ya Nachingwea kupima.
“Sina hakika kama naye atakuwa vema bila ya kupata maambukizi, maana huyu kaka yake amezaliwa mpaka anamaliza kunyonya hakupata maambukizi, alipofika miaka minne aligundulika na maambukizi ya virusi vya ukimwi,” alisema Zaituni.
Kwa mujibu wa Kaimu Mratibu wa ukimwi wilaya ya Nachingwea Dokta Khadija Komba zaidi ya watoto 458 wameambukizwa virusi vya ukimwi, pengine katika mazingira ya kuchangia nyembe, chanuo na sindano za kutolea funza na mzazi au na mzazi mwenye virusi kwa kugusuna kama ana mchubuko mwilini.
Watoto 458 waliozaliwa na mama wenye VVU, mpaka wanafikisha miezi 18 walikuwa hawana maambukizi ya virusi vya ukimwi, inawezekana wamepata maambukizi ya virusi vya ukimwi kwa kutumia vitu vya ncha kali pamoja na mama zao kwa kipindi cha miaka mitatu.
Jumla ya watoto 200 wanatumia dawa za ARVs, kati ya hao watoto wa kiume 90 na watoto wa kike 110, pia watoto 258 bado hawajaanza kutumia dawa za ARVs, kati ya hao watoto wa kiume 118 na watoto wa kike 140, kwa sababu kinga za mwili kuwa juu. Kama mtoto kinga yake ya mwili iko chini anapatiwa dawa kuanzia umri wa mwezi mmoja hadi miaka 14.
Dokta Komba alisema kuwa watoto kuanzia mwezi mmoja hadi miaka 14 wanapewa dawa aina ya AZT 390, niverapin na seprin mpaka wanapoacha kunyonya, dawa hii wanayopewa inasaidia kudumaza wadudu wa virusi vya ukimwi wasizaliene kwa wingi kwa mtoto.
Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Dokta Hussein Mwinyi, alisema kuwa mwaka 2011 jumla ya vituo 1,660 vinavyotoa huduma za (PMTCT) vilianza kutoa huduma za utambuzi kwa kutumia sampuli kwenye hospitali za rufaa.
Idadi ya watoto waliopatiwa huduma hiyo imefikia 18,231 kwa mwaka 2009 na watoto 22,033 kwa mwaka 2010 na 27, 245 kwa mwaka 2011. Kwa sasa tumefikia asilimia 26 ya kupunguza maambukizi ya virusi vya ukimwi lengo ifikapo 2015 ifikie asilia 4 ya maambukizi.
Kwa upande wake Muuguzi Mkunga anayewapima watoto wakiwa chini ya miezi 18 Evarist Chingwuile, alisema kuwa mtoto anapozaliwa na mama mwenye maambukizi ya virusi vya ukimwi anapewa dawa za AZT390 na niverapin kwa muda wa miezi 18.
Chingwuile alisema kuwa akiwa na miezi miwili anapimwa antijen katika sehemu ya unyayo kujua kama anamaambukizi au hana maambukizi, wakishamtoa damu inapelekwa katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili.
Majibu yanarudi baada ya wiki mbili, wakati wote huo mtoto anaendelea na dawa, mtoto akiachishwa kunyonya, anapimwa kumuangalia kama anamaambikizi, kama anamaambukizi anapimwa na kinga ya mwili kama iko chini anaendelea kupewa dawa ya niverpin na seprin na kumuamishi katika kituo cha ctc.
Dokta Debora Kayoka meneja wa mradi wa kumkinga mtoto asipate maambukizi kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto nchini, alisema mashine za kumpima damu ya mtoto ili kujua kama ana maambikizi au hana kwa hapa nchini, mashine hizo zipo katika hospitali za rufaa tu, kama hospitali ya Mbeya, hospitali ya Bugando, hospitali ya Kcmc na hospital ya Muhimbili.
Mashine ya (DNA-PCR) ambazo zinatumika kujua kama damu ya mtoto inamaambukizi mashine hizi zinauzwa kwa gharama ya dola ya Kimarekani 35,000 hadi dola 45,000, serikali ya Tanzania imepewa ufadhili na mfuko wa Bill Cliton Fundation.
Kwa sasa nchini Tanzania tunawataalamu wa kupima damu ya mtoto wa umri wa miezi miwili kwa kutumia mashine hii ya DNA-PCR wako wangapi 22 na wamesomea kozi za maabara Kwa muda wa miaka miaka 3, kwa kiwango cha degree,mashine hizo kwa hapa nchini zipo 10.
Chingwuile alisema kuwa kwa mwaka 2012 wanawake wajawazito waliofika kliniki kupima waliku 1,614 kati hao wasiona maambukizi ni 1565, wenye (VVU) 49, wanaume walipima na wake zao wakati wa ujauzito ni 26.
Wanaendelea na dawa ambao wana watoto wa changa ni 14. Pia mimba za utotoni 86 na wajawazito 14 wanatumia dawa hizo za kumkinga mtoto asipate na maambukizi.
Watoto wote waliozaliwa na wamama wenye virusi vya ukimwi hawana maambukizi ila mama anapojifungua salama tunamuuelekeza jinsi ya kumtunza mtoto asimuambikize virusi.
“Tunamuelimisha mama kutotumia nyembe, sabuni, sindano na chanuo pamoja na mtoto wake, anatakiwa kutunze vizuri mtoto wake kwa kumuandalia vifaa mbalimbali vya kwake kama wembe, sindano, sabuni na chanuo ili asimuambukize (VVU),” alisema Chingwuile.
Alisema kuwa baada ya miaka miwili au mitatu mama anapokuja kliniki mtoto anaanza kuumwa homa za mara kwa mara, ukimpima unamkuta mtoto amemuambukiza virusi vya ukimwi wakati alipojifungua unamuelimisha jinsi ya kumtunza mtoto ana anapokuja kliniki kila mwezi.
“Wengi husema hali ngumu ya maisha wanashindwa kununua wembe wa peke yake na mtoto akinunua wembe anatumia na mtoto wake kama kumkata kucha kumtoa funza na kumyoa nywele na kumpa vyakula akiwa chini ya miezi sita pia kunasababisha kumuambukiza virusi vya ukimwi,” alisema Mkunga Chingwuile.
Kwa upande wake mkurugenzi wa wilaya ya Nachingwea Mwanamvua Mrindoko alisema kuwa, kila mwaka wa fedha Tume ya kuthibiti ukimwi nchini wanawapatia shilingi milioni 80 kwa ajili ya mapambano ya virusi vya ukimwi laki kwa mwaka huu wa fedha mpaka sasa wamepokea shilingi milioni 20 tu bado shilingi milioni 60.
Mrindoko alisema kuwa pesa hizo wakizipata wanazitumia kwa, Kuwajengea uwezo kamati mbalimbali za ukimwi za kata. Kwa sasa wilaya ina kamati 32, pia wanawalipia ada ya shule wanafunzi waliotoka katika familia zilizoathika na ukimwi na wanafunzi wanaishi na virusi vya ukimwi na ukimwi ambao wako 438 wa shule za sekondari.
Aidha alisema kuwa zaidi ya milioni 20 inatumika kuwalipia ada wanafunzi hao wenye maambukizi ya ukimwi na ukimwi katika shule mbalimbali kuanzia kidato cha kwanza mpaka chuo kikuu.
Pia wanatoa lishe kwa wanafunzi wapata 15 wa shule ya sekondari na wanafunzi 20 wa shule ya msingi, vile vile wanatoa lishe kwa wagonjwa wenye ukimwi ambao hawajiwezi majumbani, kuwezeshwa katika miradi mbalimbali kama kutunza mazingira, kutengeneza lishe na vikoba.
Mrindoko alisema kuwa idadi kubwa ya watoto wanafunzi wanaishi na virusi vya ukimwi na wenye ukimwi katika wilaya hiyo, imetokea mwaka 1990 hadi 1998 kwa sababu kulikuwa bado hakuna dawa ya kumkinga mtoto asipate maambukizi ya virusi vya ukimwi kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto. Kwa sasa zaidi ya watu wenye 4,625 kati ya wakazi 17,00,000.
“Changamoto kubwa sana wanayoipata ni pesa kuwa finyu ukilinganisha na idadi kubwa ya maambukizi mpya ya ukimwi siku hadi siku katika msimu wa korosho na ufuta, pia uwepo wa machimbo ya madini Kiegei pamoja na makambi makubwa matatu ya kijeshi kuwepo katika wilaya hiyo na inasemekana wanajeshi hao wanafanya ngono zembe katika wilaya hiyo,”alisema Mrindoko
Kufuatia ufinyu wa bajeti na kuchelewa kufika muda muafaka, waathirika wengi hasa vijiji ambako kuna kata 26 za wilaya hiyo wanakosa huduma muhimu kama lishe na kujiunga katika vikundi vya uzalishaji mali ili waweze kujitegemea wenyewe katika kupata chakula, wanaiomba tume ya kuthibiti ukimwi nchi kuwaongea bajeti ya wilaya ya Nachingwea kutoka shilingi milioni 80 hadi ifike shilingi milioni 100.
Kwa mujibu wa kitabu kilichochapishwa kwa hisani ya Amref na Watu wa Marekani mwezi Julai mwaka 2007 na kusainiwa na Katibu Mkuu Mukama, ambacho kinaelezea muongozo kwa mama mwenye maambukizi ya virusi vya ukimwi kulimsha mtoto asiye na maambukizi , kunaweza kumuambukiza virusi hivyo.
Kitabu hicho kinaeleza kuwa mwanamke anayeishi na (VVU), anaweza kumuambukiza mtoto wake akiwa na ujauzito,uchungu na wakati wa kujifungua na wakati wa kunyonyesha.
Kama mama mjamzito hajapima (VVU), hawezi kufahamu kama anaishi na VVU. Hivyo ni muhimu wanamke mjamzito na wanaonyonyesha kupima ili kutambua hali yao ya maambukizi ya (VVU) na kupata ushauri wa jinsi ya kuwakinga watoto wao na maambukizi ya (VVU).
Mama anaishi na(VVU), damu na maziwa yake huwa na (VVU). VVU kutoka kwa mama vinaweza kwenda kwa mtoto wakati wa mimba, hususan wakati wa uchungu na kujifungua, wakati mtoto anapogusana na damu au majimaji ya mwili wa mama yeke. Ikiwa mama ananyonyesha (VVU) kwenye maziwa yake vinaweza kupita kwa mtoto.
Dokta Hussein Mwinyi alitoa ufafanuzi katika siku ya ukimwi duniani iliyofanyika katika Mkoa wa Lindi, hali halisi ya maambukizi kwa wanawake wajawazito hapa nchini kwa waka 2011, 86,875 walipatiwa dawa za ARVs kuzuiya maambukizi kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto.
Sawa na asilimia 71 ya wajawazito 122,146 waliokadiriwa kuwa na maambukizi ya virusi vya ukimwi, asilimia ya wajawazito kuwa na maambukizi ya virusi vya ukimwi imeongezeka mpaka kufikia asilimia 62 ukilinganisha na mwaka 2005 kulikuwa na asilimia 9 ya wajawazito wapatao 11,435 waliopatiwa huduma hii.
Kaimu Mganga mkuu wa Wilaya dokta John Sijaona alisema kuwa, tatizo la watoto wa chini ya miaka 15 kupata maambukizi linatokana na elimu duni kwa wanawake wanaoishi na virusi vya ukimwi pamoja na ugumu wa maisha mama anashindwa kutenga vifaa mbalimbali vya kutumia mtoto wake na kusababisha kumuambukiza virusi vya ukimwi.
“Mama akipewa elimu ya kutosha jinsi ya kumtunza mtoto aliyemzaa asimuambukize virusi vya ukimwi itasaidia kupunguza maambukizi kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto, lakini ugumu wa maisha nao unachangia mama kushindwa kumudu kununua nyembe, chanuo na sindano kwa mtoto pekee,” alisema Dokta Sijaona
Makala ya kisayansi iliyofanywa na dokta Kahabi Isangura mwaka 2007-2008 ambaye pia ni mtaalamu wa afya ya jamii inasema kuwa, kiwango cha maambukizi kwa wanawake ni asilimia 21.5 na wanaume kiwango cha maambukizi ni asilimia 11.4.
Makala hiyo ya kisayansi inaeleza kuwa kati ya watoto 70,000 hadi 80,000 wanaozaliwa kila mwaka wapo hatarini kuambukizwa virusi vya ukimwi (VVU) kipindi cha kuzaliwa na wakati wa kunyonya.
Kipindi cha mwaka 2007-2008 zaidi ya watu milioni 1,400,000 wanaishi na virusi vya ukimwi, kati hao wanawake ni asilimia 52 na asilimia 11. 4 ni watoto wa chini ya umri wa miaka 15.
Aidha makala hiyo inaeleza kuwa kwa sasa Tanzania inakadiliwa kuwa na watu milioni 2, 113,158 wanaishi na virusi vya ukimwi lakini kati ya hao asilimia 21. 5 ndio wanaopatiwa dawa za kupunguza makali ya ugonjwa huo.
Sunday, April 21, 2013
Friday, April 19, 2013
NGONO ZEMBE YA WANAFUNZI KIJIJINI KIEGEI KWA BEI YA 500
Hii
ndio hali halisi utakayo kutana nayo kilometa 660 kutoka Dar es Salaam na
kilimeta 122 kutoka Nachingwea. Katika kijiji cha Kiegei kila tarehe 25 ya
mwisho wa mwezi, baada ya mnada wa bidhaa mbalimbali za kilimo kama chakula na
vifaa vya nyumbani kama vyombo.
Watu
wengine, wekiwemo watoto wa shule za msingi huuziana mabusu na wafanyabiashara
wa mnada huo, kusababisha kukatisha masomo kwa baadhi ya wanafunzi kwa kushika
ujauzito na wengine kupata magonjwa ya
kuambukiza kama gono, kaswende na Ukimwi.
Baada
ya kuuza bishaa zao mbalimbali katika mnada
huo, unaohusisha wafanyabiashara kutoka katika wilaya za jirani kama
Liwale, Tunduru na Masasi, wafanyabiasha wa Kiegei huingia katika vibanda vya
sinema, mathalani kuangalia filamu mbalimbali, lakini humo ndani ya vibanda
filamu hutumia pesa zao kununua ngono kutoka kwa watoto.
Sera
ya Maendeleo ya Mtoto ya mwaka 2008 inalenga kuhakikisha kwamba watoto wote
wanastawi na kuwa na maisha bora, kutokana na kupatikana kwa haki zao za msingi
ambazo ni kuishi, kuendelezwa, kulindwa na kushirikishwa katika mambo
yanayowahusu bila ua ubaguzi wa hali yoyote.
Kwa
mujibu wa sera hiyo, mtoto ni yule mwenye umri wa chini ya miaka 18. Mtu yeyote
mwenye umri wa chini ya miaka 18 anastahili kulindwa na familia yake pamoja na
wanajamii wanaomzunguka ili kumuangalia ukuaji wake uwe wenye usalama zaidi.
Madhara
ambayo anaweza kuyapata mtoto kama hajapata uwangalizi kutoka katika familia
yake na jamii inayomzunguka ni, kuathirika kiafya, kiakili, kimwili, kihisia na
kijinsia.
Pia
pale ambapo maendeleo ya mtoto yanavurungwa, ni pale uhai wa mtoto uko
hatarini pamoja na utu wa mtoto unapokosekana.
Sheria
ya kimataifa ya mwaka 2009 ya kutetea watoto kutoka umoja wa mataifa inaeleza
kuwa, mtoto wa chini umri wa miaka 18 anatambulika kama mtoto kidunia na
anastahili kulindwa na familia yake na kupewa mahitaji muhimu kama chakula
bora, maradhi, nguo na elimu bora, mtoto huyu atakiwa kuanza kujitegemea yeye
mwenyewe au kuachiwa huru kufanya ngono zembe na ajira majumbani na mashambani
ili alishe familia hairuhusiwi kimataifa.
Lakini,
ukitembelea vibanda vya sinema vya kijiji cha Kiegei kuanzia saa 12.00 jioni,
utawakuta watoto wa kike, wenye umri kuanzia 10 hadi 14, katika shuguli mbali
mbali za kutafuta hela kwa kuuza ngono.
Siku
ya tarehe 25 Januari, 2013, ambayo ilikuwa ni siku ya ijumaa, zikioneshwa
sinema za kivita mbili, wasichana wapatao 10 walionekana ndani ya kibanda cha
sinema kilichopo katika kijiji cha Kiegei, wakipakwatwa na kushikwa-shikwa na
wanaume wenye umri mkubwa.
Saa
6:00 usiku, kila mtoto alitoka na mwanaume na kuelekea sehemu mbalimbali kama
vyoo vya shule ya msingi Kiegei, uwanja wa mpira na wengine kwenye meza za
mchezo wa pool, iliyopo katika Soko dogo la kijiji cha Kiegei na wengine
pembezoni mwa jengo la Kanisa.
Mtoto
huyo na mwanaume mtu mzima wakiwa katika meza ya mchezo wa pool, wakaanza
kufanya ngono mbele ya macho yangu, bila hata ya kuona aibu yoyote, tena bila
hata huruma kama anayefanya naye ngono ni mtoto wa shule ya msingi.
“Kama unaona mwenzio anafaidi na tendo hili la
ngono basi njoo weye mtu mzima ufanye; naona umeshangaa kwa kutoa macho
utazani hujui nini kinachofanyika hapa,” alisema jibaba hilo huku akiendelea
kufanya ngono na kitoto hicho.
Saa
12:00 asubuhi kesho yake, hakukukuwa na mabaki ya kondom katika maeneo haya
yote.
Kwa
mujibu wa wanafunzi wa shule ya msingi Kiegei, wanalipwa kiasi cha sh.500 hadi
sh.2000 kufanya ngono na watu wazima.
“Nimeanza
ngono nikiwa na umri wa miaka 12, kabla hata sijabalehe nafanya ngono na
wanaume wakubwa ambao ni wachimbaji wa madini Mbwemkuru na wafanyabiasha ya
mnada wanaofika kila tarehe 25 ya mwisho wa mwezi, kwa ujila wa Tshs. 500 hadi
Tshs. 2000 kwa siku,” alisema Anna Peter (13) sio jina lake
Wakati
huo huo, mwalimu mkuu wa shule ya Kiegei, Fred Mchekenje, alisema kuwa
wanafunzi wa shule yake bado hawajaanza kufanya ngono kwani bado wadogo sana na
kudai kwamba mambo hayo wanafanya watoto wa mitaani.
“Bado
wadogo sana; hawajaanza kufanya mambo hayo ya kiutu uzima. Wanapenda kusoma na
muda mwingi wako nyumbani wanajisomea wakitoka shuleni,” alisema
Mchekenje.
Mchekenje
alisema kuwa, mwaka 2012 wanafunzi wapatao 29, walifanya mtihani wa kumaliza darasa
la saba, kati ya hao wanafunzi 29 walifaulu kujiunga na kidato cha kwanza
katika shule ya sekondari Kiegei, kati ya hao wasichana 11 na wavulana 18.
Mwaka
2011 wanafunzi walifaulu walikuwa asilimia 70 na wakapata fulsa ya
kujiunga na masoma ya sekondari na vyuo vya ufundi stadi veta.
Asilimia
30 ndio waliobaki mtaani ambao hawakufaulu na kupata nafasi ya kuendelea na
masomo ya sekondari katika shule mbalimbali za sekondari Nachingwea.
Aidha
alisema kuwa matokeo ya darasa la nne yalikuwa mabaya sana kwa mwaka 2012;
waliofanya mtihani walikuwa 95 na waliofaulu ni watoto nane tu. Kati ya hao,
wavulana walikuwa sita na wasicha ni wawili. Kwa mujibu wake, sababu kubwa ya
kufeli ni kutokuwepo kwa vitabu, chaki na upungufu wa walimu; badala ya 15, kwa
sasa wapo watatu.
Mchekenje
alisema kuwa mahudhurio ya watoto wa kike shuleni ni mazuri na hakuna mimba
iliyopatikana kwa miaka saba sasa; mara ya mwisho kumpata mtoto mwenye ujauzito
ni mwaka 2006. Anadhani sababu kubwa ya kupungua kwa mimba shuleni ni kuwepo
kwa somo la elimu lika lililoanza kufundishwa mwaka 2007.
Kwa
mujibu wa Juma Ramadhani, ambaye ni mkazi wa kijiji hicho na mzazi wa watoto
watatu wanasoma katika shule ya msingi Kiegei, mwaka 2012, wanafunzi wawili
walipata mimba wakiwa darasa la sita na kukatisha masomo yao.
Kama
Anna, Salima Musa (sio jina lake) ni mwanafunzi wa shule ya msingi. Mtoto huyu,
amabye ana miaka 11 na yuko darasa la tano katika shule ya msingi Ukombozi
anasema, “Nimezoeya kufanya ngono na watu wazima. Sitaki watoto wa shule
wenzangu kwa sababu wananuka mkojo; nataka wanaume wenye misuri iliyokomaa
kwani ndio nasikia raha zaidi.”
Aziza
Ally (siyo jina lake) aliacha shule mwaka huu, akiwa darasa la sita. Hana ndoto
tena za kwenda shule maana ngono anayofanya ndio inampa uwezo wakuilisha
familia yake kwa sasa.
“Sijawahi
kutumia kondom toka nimeanza kufanya ngono nikiwa darasa la nne. Kwa sasa
nimeamua kuacha shule kwa sababu walimu wameniamba nirudie darasa la tano
badala ya kuwa darasa la sita.
Nimeona bora nifanye ngono ili nijikimu kimaisha
kwa kujinunulia nguo, viatu na mafuta mazuri pamona na kutoa nyumbani pesa ya
chakula. Hapa unaponiona nimetoka kumaliza dozi ya ugonjwa wa gono wiki
moja iliyoisha na sasa niko mawindoni natafuta pesa.”
Baba
yake Aziza aliki kufahamu kwamba mtoto wake anajihusisha na ngono zembe.
“Nimemkanya
asifanye ngono lakini hasikii. Nimeamua kumuacha tuu ila kwa sasa sina huduma
yoyote ninayopa mtoto huyo; anajinunulia mwenyewe nguo za kuvaa, mafuta ya
kupaka na chakula,”alisema Baba yake Aziza.
Kwa
mujibu wa Dk. Kahabi Isangura, mtaalamu wa magonjwa ya kijamii, kuna madhara
makubwa sana kwa mtoto kuanza kufanya ngono katika umri mdogo. Anaweza kupata
mimba na kukatisha ndoto zake za kusoma, anaonekana muhuni pamoja na kukabiliwa
na majukumu makubwa akiwa na umri mdogo.
Dk.
Isangura alisema kuwa madhala ya kiafya ni kama kupata magonjwa ya kuambukiza
yakiwemo ukimwi, gono, kaswende na kisonono. Pia, anaweza kupata kansa ya
kizazi kwa kuanza ngono mapema kwa sababu seli za kingo za uke zinakuwa
hazijakomaa vema, hivyo nirahisi kupata majereha na kuweka ufa ambao
unasababisha kupata kansa ya kizazi akiwa mtu mzima.
Ngono
ya utotoni husababisha vifo vya wajawazito wakati wa kujifungua kwa sababu
mtoto mwenye umri wa chini ya miaka 14 nyonga yake ya uzazi inakuwa bado
haijakomaa kusukuma mtoto wakati wa kujifungua, hivyo basi kunauwezekano mkubwa
wa mtoto huyu kupoteza maisha wakati wa kujifungua.
Kwa
mujibu wa takwimu zilizotolewa na Mganga wa Zahanati ya Kiegei Olafu Chinguile,
mwaka 2011 wagonjwa 48 walifika wakiwa wanaumwa magonjwa ya Kaswende na Gono;
kati ya hao watoto walikuwa 5.
Mwaka
2012 wagonjwa waliofika katika zahanati yake wakiwa wanaumwa magonjwa ya Gono
na Kaswende walikuwa 38; kati ya hao, nane walikuwa watoto kati ya miaka 10 na
14.
Habiba
Juma alimaliza darasa la saba katika shule ya msingi kiegei mwaka 1994 na
kusema kuwa, kipindi alichokuwa anasoma yeye hakukuwa na mambo ya ngono kwa
wanafunzi na watu wazima, lakini ilipofika mwaka 1995 ndio mambo ya ngono kwa
wanafunzi yalipoanzia baada ya kuanza kwa machimbo ya madini.
Makwasa Bulenga ni
Afisa elimu wa shule ya msingi wilaya ya Nachingwea alisema kuwa,tatizo kubwa
la wanafunzi kufanya ngono ni kuwepo kwa vibanda vya kuonesha sinema mbalimbali
muda wa usiku.
“Vibanda
vya sinema kwa vijijini ndio tatizo kubwa kwa watoto wa shule ya msingi
kujifunza mambo machafu, huku sinema hizo wakiangalia na watu wazima tena
wanaume hasa wachimbaji wa kutoka sehemu mbalimbali za uchimbaji,”alisema
Bulenga
Bulenga
alisema kuwa ofisi yake imewaita mara kadhaa viongozi wa vitongoji na vijiji
kuwaeleza umuhimu wa vibanda vya sinema kufungwa mapema, lakini juhudi hizo
zimegonga mwamba kwa sababu vibanda hivyo vinaanza kuonesha sinema kuanzia saa
12:00 jioni hadi saa 6:00 usiku na wateja wao wakubwa ni watoto wa shule za
msingi.
Vibanda
vya sinema vinatakiwa kuanza kuonesha sinema saa 8:00 mchana hadi saa 12:00
jioni.
“Sio
tuu kiegei watoto kufanya ngono; na vijiji vingine pia hali ni hiyo hiyo kama
uliyoishudia kiegei, bado tupo katika hali mbaya sana kwa watoto kuanza ngono
mapema kwa wilaya ya Nachingwea,” alisema Bulenga.
Kwa
mujibu wa Bulenga, katika wilaya ya Nachingwea kuna kata 32; kati ya hizo, kata
sita pekee ziko mjini. Nyingine zote ziko vijijini na sehemu kubwa yake ndio
kuna wanafunzi wengi ambao wanafanya ngono baada ya kumaliza kuangalia sinema
za ngono katika maeneo hayo.
Mjini
kuna wanafunzi wapatao 4,789; wavulana ni 2,365 na wasichana 2,424. Vijijini
kuna wanafunzi 27,047; kati yao,
wavulana wako 13,319 na wasichana ni 13,728. Walimu waliopata mafunzo
kuhusu somo la elimu lika kwa wilaya ya Nachingwea wako 23; wanaume 14 na
wanawake9.
Inapaswa
kuwa na walimu ambao wamepatiwa elimu lika 300, ili kiweza kukidhi idadi ya
wanafunzi wa shule za mjini na vijijini katika wilaya ya Nachingwea kwa sasa.
Walimu
ambao hawakupata mafunzo lakini wanafundisha somo hilo la elimu lika wako 200;
wanaume 116 na wanawake 84. Hii inachangia uwajibikaji mdogo kwa walimu ambao
hawajapatiwa mafunzo ya somo hilo jinsi ya kumfundisha mwanafunzi akajiepusha
na ngono.
Kwa
upande wake, Jane Mrema mshauri wa masuala ya jinsia na kutetea haki za
watoto na vijana kutoka Plan International alisema kuwa, tatizo la shule ya
msingi Kiegei kwa watoto kuanza ngono halifahamu.
Mrema
alisema kuwa watoto wanalengwa na shirika la Plan International ni kuanzaia
mwezi mmoja mpaka miaka 18, hasa kwa watoto wa kike pamoja na walemavu. Kwa
sasa wanafanya kazi katika mikoa mitano nayo ni Mwanza, Geita, Morogoro, Pwani
na Dar es salaam lakini pia wanafanya katika wilaya sita ambazo ni Kibaha,
Kisarawe, Kilombero, Sengerema, Ilemela, Geita na Ilala.
“Tunamuelisha
mtoto wa kike kutambua haki yake ya kupata elimu bora na afya bora, pia mtoto
kufahamu unyanyasaji wa kijinsia majumbani na njiani akienda shuleni,
pamoja na kuangalia mazingira ambayo yapo hatarishi kwa kupata unyanyasaji wa
kijinsia kwa mtoto wa kike,” alisema Mrema.
Aidha
Plan International wamejenga mabweni katika wilaya mbalimbali kama Ilala katika
shule ya sekondari sakara, kibaha shule ya sekondari ya ruvu, mwanza na
geita kila bweni linauwezo kuchukua watoto 100, pia wamejanga choo na mabomba
ya maji safi.
Kwa
sasa kuna kampeni nyingine ijulikanayo kama kwa sababu mimi ni msichana
ambayo lizinduliwa mwishoni mwezi wa Octoba mwaka jana, lengo kubwa la kampeni
hii ni, kuhamasisha jamii kutetea haki za mtoto wa kike kwa sababu watoto wa
kike ndio waathirika wakubwa.
Kampeni
hii ilikuwa na ujumbe usemao maisha yangu, haki yangu tokomeza ndoa za utotoni,
kampeni hii hasa inajikita kumtetea mtoto wa kike kuepukana na unyanyasaji wa
kijinsi na kupata haki zake za msingi na elimu bora.
Pia
wamejikita katika suala la afya ya uzazi kwa watoto wa kike, kwa kuwajengea
uwezo kujilinda na kujitunza na kufikia ujana vizuri, pia kutokomeza mira
potofu kama ukeketaji na ndoa za utotoni.
Wednesday, April 17, 2013
NAPENDA KUSOMA
Kituo hicho kipo Goba Umoja Manispaa ya Kinondoni mkoa wa Dar es Salaam. Sababu kubwa ya kuwa na vitu hivi ni kutokana na eneo hili kuwa mbali na zahati ya Goba, kwa hiyo inakuwa ngumu kwa akinamama kuwapeleka kupima watoto kila mwezi. Kituo hicho kimewapima watoto wa chini ya miaka 5 wapatao 50 kwa siku ya leo.
Tuesday, April 16, 2013
WAJAWAZITO NA WATOTO MSAKUZI KINONDONI BADO WANAPIMWA CHINI YA MTI MKAMVU
Kutoka katika mti mkavu huo, ambao unatumika kupima watoto wa chini ya miaka mitano na wajawazito kwa miaka miwili, katika eneo la Msakuzi mtaa wa Ruguruni katika kata ya Kwembe wilaya ya Kinondoni. Mpaka kuingia katika jengo ndogo la kliniki lililojengwa kwa ufadhili wa mfuko wa Jimbo la Ubungo.
Akinamama wakiwa na watoto wao walikuwa wakinyeshewa mvua na kuchomwa na jua kali. Adha hiyo inawapata kwa kufuata huduma ya vipimo mbalimbali, kwa wajawazito na watoto wao katika mti huo mkavu.
Kwa sasa adhabu hiyo itaanza kusahaulika kwa kujengewa jengo ndogo, la vyumba vitatu ambalo litakuwa linatumika kwa upimaji wa watoto na wajawazito.
Lakini sio tu kuwapima bali, hata kujifungua katika jengo hilo ambalo lililojengwa kwa ufadhili wa mfuko wa jimbo. Kwa zaidi ya mwaka mmoja na miezi sita sasa, toka Mbunge wa Jimbo la Ubungo John Mnyika kufungua jengo hilo, mpaka sasa bado halijaanza kutoa huduma bado akimama wanaendelea kutaabika kwa kuendelea kupimwa katika mti huo.
Mganga Mkuu wa wilaya ya Kinondoni Dk. Gunini Kamba akimkabidhi vifaa mbali mbali vya jengo hilo, Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi tawi la Msakuzi Leard Kitunga.
Dk. Kamba alisema kuwa, amesikia kilio cha wanawake wa Kwembe juu ya tatizo hilo, la kuwapima wajawazito chini ya mti na watoto kwa muda wa miaka miwili.
"Tumesikia kilio cha wajawazito na mama wenye watoto wadogo, wanaonyeshewa mvua na kuchomwa na jua, kwa kukosa jengo pamoja na vifaa na wahudumu, leo tumewaletea vitanda vitatu, kimoja kwa ajili ya kujifungulia na vitanda viwili vya kawaida, mzani wa kupimia watoto na mzani wa kupimia watu wazima na Makintoshi mita 25 ambayo inatumika kutandikia katika kitanda cha kujifungulia,"alisema Dk. Kamba.
Dk. Kamba alisema kuwa vifaa hivyo walivyowakabidhi siku ya leo katika kituo hicho cha kutoa huduma ya kupima na kujifungua, kitasaidia kutoa huduma ya wajawazito na watoto katika eneo hilo, ambalo akina mama wamekuwa wakitumia gharama kubwa kufuata huduma hiyo katika hospitali ya Mwananyamala, Tumbi Kibaha na Sinza.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi wa tawi hilo Kitunga alisema kuwa, wanamshukuru Dk. Kamba kwa kuwasikia kilio chao cha muda mrefu kwa kuwapelekea vifaa hivyo vya msingi, kwa ajili ya upimaji wa wajawazito, kujifungu na upimaji wa watoto.
"Tunamshukuru sana Dk. Kamba kwa kujali na kuguswa na suala la matatizo ya wajawazito na watoto katika eneo hili la Msakuzi, tunamuomba asisahau kutuletea muuguzi na nesi katika kituo hiki ili huduma ianze kwa kuwapunguzia adha wakazi wa Kwembe,"alisema Kitunga.
Rafail Maria mkazi wa eneo hilo alisema kuwa, kuletwa kwa vifaa hivyo katika kituo hicho kidogo cha upimaji, itasaidia kupunguza usumbufu wa kwenda mbali na kunyeshewa na mvua na kuchomwa na jua kwa watoto na wajawazito, wanaofika kila mwisho wa mwezi kupima na kupatiwa chanjo.
Jannet Liytuu (36) ni mama mwenye watoto watatu, kwa sasa anamtoto mwenye miezi nane naye anapima katika mti huo mkavu siku ya kliniki, kwa sababu ya jengo hilo toka limezinduliwa hakuna vifaa wala muuguzi.
"Nimejifungulia katika hospitali ya Mwananyamala, kwa sababu hakuna zahanati wala kituo cha afya katika eneo hili, basi unatakiwa kwenda Mwananyamala maana ukienda hospitali ya Tumbi unarudishwa hata ukiwa unaumwa uchungu wanakataa kukupokea,"alisema Liytuu.
Aidha ukitaka huduma ya wajawazito na watoto inakulazimu kwenda mabwepande na Kibamba ambako, ni lazima uvuke mito miwili ili ufike katika zahanati ya Kibamba kama mto wa Kibwegere na Mdidimu, mito hii ikijaa maji hakupitiki kiurahisi kwa sababu hakuna madajara.
Anastazia Mwakalinga (37) mkazi wa eneo la Msakuzi amajifungua miezi miwili iliyopita katika hospitali Tumbi Kibaha, alipata shida sana kwa sababu alipofika katika hospitali hiyo, akiwa anaumwa uchungu waligoma kumsaidia kujifungua, mpaka alipokwenda katika zahanati mmoja ya wilaya ya Kibaha kumuandikia kwenda kujifungulia hospitali yaTumbi, alipofika Tumbi alijifungua mtoto aliyefariki kwa sababu alichukua muda mwingi kupata karatasi ya maelekezo ya kujifungua hapo.
"Kituo hiki kingekuwa na vifaa na muuguzi ningejifungulia hapa na wala nisingehangaishwa nilipofika katika hospitali ya Tumbi, na wala mtoto wangu asingefikia hatua ya kupoteza maisha kwa kuchelewa kupata huduma ya kujifungua,"alisema Mwakalinga.
Dk. Kamba alisema, Kwa sasa wamepata eneo la heka kumi katika kata ya Kibamba, mtaa wa Hondogo kwa Neema, kwa kujenga kituo kikubwa cha afya ambacho kitatoa huduma kwa wakazi wa kata, Kwembe, Kibamba, Msigani, Mbezi, Kimara na Saranga.
Kwa sasa wako katika fidia ya kuwalipa wakazi wa eneo hilo, malipo ambayo ni zaidi ya shilingi milioni 100, aidha eneo la Msakuzi lina kaya zipatazo 1,000, kaya zote hizo zinategemea kupata huduma ya afya katika kata ya Kibamba na Mabwepande. Gharama za kukodi tax kwenda hospitali ya Mwananyamala ni shilingi 400,000, hospitali ya Sinza ni shilingi 30,000, hospitali ya Tumbi shilingi 20,000.
Uwajibikaji wa aina hii ni kama wa Dk. Kamba, katika kuhakikisha wajawazito na watoto wanapata huduma bora sehemu wanakoishi, ndio unaohitajika kwa watendaji mbalimbali hapa nchini.
Kama tunajali na kuguswa na changamoto mbalimbali zinazohusu masuala ya wajawazito na watoto, vifo vya kizembe haviwezi tena kuendelea kutokea kwa sababu, kila mmoja anajua wajibu wake na nini cha kufanya ili kuweza kupunguza vifo vya wajawazito hapa nchini.
Lakini Dk. Kamba amejitahidi kupeleka vifa hivyo katika kituo kidogo cha kupima wajawazito na watoto, bado anahitajika muuguzi na nesi kuweza kutoa huduma hiyo kwa walengwa wa eneo la Msakuzi na maeneo jira, usichoke pambana ili uweze kumpata muuguzi na nesi mwenye kiwango cha juu katika kutoa huduma kwa Msakuzi, hiyo ndio kazi uliopewa na Mwenyezi Mungu ya kuwaokoa wajawazito na watoto wa chini ya miaka mitano.
Akinamama wakiwa na watoto wao walikuwa wakinyeshewa mvua na kuchomwa na jua kali. Adha hiyo inawapata kwa kufuata huduma ya vipimo mbalimbali, kwa wajawazito na watoto wao katika mti huo mkavu.
Kwa sasa adhabu hiyo itaanza kusahaulika kwa kujengewa jengo ndogo, la vyumba vitatu ambalo litakuwa linatumika kwa upimaji wa watoto na wajawazito.
Lakini sio tu kuwapima bali, hata kujifungua katika jengo hilo ambalo lililojengwa kwa ufadhili wa mfuko wa jimbo. Kwa zaidi ya mwaka mmoja na miezi sita sasa, toka Mbunge wa Jimbo la Ubungo John Mnyika kufungua jengo hilo, mpaka sasa bado halijaanza kutoa huduma bado akimama wanaendelea kutaabika kwa kuendelea kupimwa katika mti huo.
Mganga Mkuu wa wilaya ya Kinondoni Dk. Gunini Kamba akimkabidhi vifaa mbali mbali vya jengo hilo, Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi tawi la Msakuzi Leard Kitunga.
Dk. Kamba alisema kuwa, amesikia kilio cha wanawake wa Kwembe juu ya tatizo hilo, la kuwapima wajawazito chini ya mti na watoto kwa muda wa miaka miwili.
"Tumesikia kilio cha wajawazito na mama wenye watoto wadogo, wanaonyeshewa mvua na kuchomwa na jua, kwa kukosa jengo pamoja na vifaa na wahudumu, leo tumewaletea vitanda vitatu, kimoja kwa ajili ya kujifungulia na vitanda viwili vya kawaida, mzani wa kupimia watoto na mzani wa kupimia watu wazima na Makintoshi mita 25 ambayo inatumika kutandikia katika kitanda cha kujifungulia,"alisema Dk. Kamba.
Dk. Kamba alisema kuwa vifaa hivyo walivyowakabidhi siku ya leo katika kituo hicho cha kutoa huduma ya kupima na kujifungua, kitasaidia kutoa huduma ya wajawazito na watoto katika eneo hilo, ambalo akina mama wamekuwa wakitumia gharama kubwa kufuata huduma hiyo katika hospitali ya Mwananyamala, Tumbi Kibaha na Sinza.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi wa tawi hilo Kitunga alisema kuwa, wanamshukuru Dk. Kamba kwa kuwasikia kilio chao cha muda mrefu kwa kuwapelekea vifaa hivyo vya msingi, kwa ajili ya upimaji wa wajawazito, kujifungu na upimaji wa watoto.
"Tunamshukuru sana Dk. Kamba kwa kujali na kuguswa na suala la matatizo ya wajawazito na watoto katika eneo hili la Msakuzi, tunamuomba asisahau kutuletea muuguzi na nesi katika kituo hiki ili huduma ianze kwa kuwapunguzia adha wakazi wa Kwembe,"alisema Kitunga.
Rafail Maria mkazi wa eneo hilo alisema kuwa, kuletwa kwa vifaa hivyo katika kituo hicho kidogo cha upimaji, itasaidia kupunguza usumbufu wa kwenda mbali na kunyeshewa na mvua na kuchomwa na jua kwa watoto na wajawazito, wanaofika kila mwisho wa mwezi kupima na kupatiwa chanjo.
Jannet Liytuu (36) ni mama mwenye watoto watatu, kwa sasa anamtoto mwenye miezi nane naye anapima katika mti huo mkavu siku ya kliniki, kwa sababu ya jengo hilo toka limezinduliwa hakuna vifaa wala muuguzi.
"Nimejifungulia katika hospitali ya Mwananyamala, kwa sababu hakuna zahanati wala kituo cha afya katika eneo hili, basi unatakiwa kwenda Mwananyamala maana ukienda hospitali ya Tumbi unarudishwa hata ukiwa unaumwa uchungu wanakataa kukupokea,"alisema Liytuu.
Aidha ukitaka huduma ya wajawazito na watoto inakulazimu kwenda mabwepande na Kibamba ambako, ni lazima uvuke mito miwili ili ufike katika zahanati ya Kibamba kama mto wa Kibwegere na Mdidimu, mito hii ikijaa maji hakupitiki kiurahisi kwa sababu hakuna madajara.
Anastazia Mwakalinga (37) mkazi wa eneo la Msakuzi amajifungua miezi miwili iliyopita katika hospitali Tumbi Kibaha, alipata shida sana kwa sababu alipofika katika hospitali hiyo, akiwa anaumwa uchungu waligoma kumsaidia kujifungua, mpaka alipokwenda katika zahanati mmoja ya wilaya ya Kibaha kumuandikia kwenda kujifungulia hospitali yaTumbi, alipofika Tumbi alijifungua mtoto aliyefariki kwa sababu alichukua muda mwingi kupata karatasi ya maelekezo ya kujifungua hapo.
"Kituo hiki kingekuwa na vifaa na muuguzi ningejifungulia hapa na wala nisingehangaishwa nilipofika katika hospitali ya Tumbi, na wala mtoto wangu asingefikia hatua ya kupoteza maisha kwa kuchelewa kupata huduma ya kujifungua,"alisema Mwakalinga.
Dk. Kamba alisema, Kwa sasa wamepata eneo la heka kumi katika kata ya Kibamba, mtaa wa Hondogo kwa Neema, kwa kujenga kituo kikubwa cha afya ambacho kitatoa huduma kwa wakazi wa kata, Kwembe, Kibamba, Msigani, Mbezi, Kimara na Saranga.
Kwa sasa wako katika fidia ya kuwalipa wakazi wa eneo hilo, malipo ambayo ni zaidi ya shilingi milioni 100, aidha eneo la Msakuzi lina kaya zipatazo 1,000, kaya zote hizo zinategemea kupata huduma ya afya katika kata ya Kibamba na Mabwepande. Gharama za kukodi tax kwenda hospitali ya Mwananyamala ni shilingi 400,000, hospitali ya Sinza ni shilingi 30,000, hospitali ya Tumbi shilingi 20,000.
Uwajibikaji wa aina hii ni kama wa Dk. Kamba, katika kuhakikisha wajawazito na watoto wanapata huduma bora sehemu wanakoishi, ndio unaohitajika kwa watendaji mbalimbali hapa nchini.
Kama tunajali na kuguswa na changamoto mbalimbali zinazohusu masuala ya wajawazito na watoto, vifo vya kizembe haviwezi tena kuendelea kutokea kwa sababu, kila mmoja anajua wajibu wake na nini cha kufanya ili kuweza kupunguza vifo vya wajawazito hapa nchini.
Lakini Dk. Kamba amejitahidi kupeleka vifa hivyo katika kituo kidogo cha kupima wajawazito na watoto, bado anahitajika muuguzi na nesi kuweza kutoa huduma hiyo kwa walengwa wa eneo la Msakuzi na maeneo jira, usichoke pambana ili uweze kumpata muuguzi na nesi mwenye kiwango cha juu katika kutoa huduma kwa Msakuzi, hiyo ndio kazi uliopewa na Mwenyezi Mungu ya kuwaokoa wajawazito na watoto wa chini ya miaka mitano.
Monday, April 15, 2013
SAKATA LA ARVs BANDIA, SERIKALI ITOE TAARIFA SAHIHI KULINDA AFYA ZA WATUMIAJI
Tumesikitishwa kupata taarifa kwamba watu 5,358 wanaoishi na Virusi vya UKIMWI (VVU) waliokuwa kwenye matibabu wameacha kutumia dawa za kupunguza makali ya ugonjwa huo (ARVs), mkoani Dodoma.
Taarifa kupitia vyombo vya habari na taasisi mbalimbali kuhusu Watu wanaoishi na Virusi vya UKIMWI (WAVIU) kuacha kutumia dawa, zimekuja kipindi ambacho wananchi na wadau wa UKIMWI wakitafakari hatma ya uchunguzi wa sakata la kutengenezwa dawa bandia za ARVs. Dawa hizo aina ya TT-VIR toleo namba (batch number oc.01.85) zilisambazwa katika mikoa ya Mara, Tanga na Dar es Salaam tangu Mei, 2011.
Kuwepo kwa ARVs bandia na taarifa juu ya WAVIU kuacha kutumia dawa kunadhihirisha udhaifu uliopo ndani ya mifumo na mamlaka za serikali zilizopewa kusimamia ubora, uwepo na upatikanaji wa dawa. Sikika inaamini, pengine kuna uhusiano wa karibu kati ya uwepo wa dawa hizo bandia nchini na WAVIU hao kuingiwa hofu na kuacha kutumia dawa.
Tunaamini hayo kwa kuzingatia ukweli kwamba suala la mgonjwa kutumia dawa kwa kiasi kikubwa linategemea imani na utayari wa mhusika. Uwepo wa dawa bandia ama zisizo na ubora unapunguza imani na hivyo kuweza kusababisha mgonjwa kuacha kuzitumia na kupelekea kuathirika zaidi.
Sakata la kuwepo kwa ARVs bandia lililochukua takribani miezi nane sasa, limekuwa na sura tofauti hususan juu ya nani anahusika moja kwa moja baada ya kiwanda kinachodaiwa kutengeneza dawa hizo Tanzania Pharmaceticals Industry (TPI) kukanusha kuhusika na utengenezaji huku Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) na Bohari Kuu ya Dawa (MSD) wakisisitiza kuwa dawa hizo zimetoka kiwandani hapo.
Sikika inathamini na kutambua juhudi za serikali za kutekeleza taratibu za kisheria ikiwemo ukaguzi na uchunguzi wa kimaabara uliofanywa na Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii kupitia TFDA. Hatua nyingine iliyochukuliwa na serikali ni kukifungia kiwanda cha TPI kutokana na nyaraka zilizokutwa MSD kuonesha kuwa TPI iliiuzia MSD dawa hizo. Serikali pia iliwasimamisha kazi watendaji watatu wa MSD.
Usambazaji na matumizi ya dawa aina ya TT –VIR 30 toleo namba 0C .01.85 pia ulipigwa marufuku na serikali ilizitaka mamlaka za serikali za mitaa kupitia waganga wakuu, kukusanya dawa hizo bandia kutoka vituo vya huduma za afya na kwa wananchi, na kisha kuzirudisha MSD.
Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa na MSD, takribani makopo 8,000 ya toleo hilo kati ya zaidi makopo 12,000 yaliyosambazwa yalikusanywa. Hivyo kwa hesabu rahisi, kuna takribani makopo 4,000 ambayo bado yapo kwenye mzunguko na ambayo hakuna taasisi yenye uhakika wa yalipo makopo hayo; kwenye vituo vya huduma ama kwa wananchi.
Serikali ililifikisha suala la ARVs bandia kwa Mkurugenzi wa Makosa ya Jinai (DPP) kwa uchunguzi na hatua zaidi za kisheria. Lakini, pamoja na juhudi hizo za serikali, Sikika hairidhishwi na kasi ndogo ya ufuatiliaji wa tatizo hilo hususan muda mrefu unaotumika kupeleleza.
Kwa mujibu wa taarifa kutoka ofisi ya DPP, jalada la kesi ya ARVs bandia limepokelewa na linashughulikiwa ili kupata muelekeo wa nani ahusishwe na kwa kosa gani kabla ya kuachia mamlaka husika jukumu la uchunguzi wa kina. Kwa maelezo ya ofisi hiyo, suala la ARVs bandia limechukua muda mrefu (zaidi ya miezi miwili), tofauti na muda wa kawaida wa siku 14 unaotumiwa na ofisi ya DPP kushughulikia kesi mbalimbali zinazofikishwa hapo, kutokana na uzito/unyeti wa suala hilo.
Wakati taratibu hizo za kitaalamu na kisheria zikiendelea, tunaishauri serikali kutoa taarifa rasmi kwa wananchi juu ya dawa bandia (makopo 4,000) ambazo hazijakusanywa. Je, ziko vituoni au zilishatumiwa na wananachi? Kama zilishatumiwa, je serikali ina taarifa zozote juu ya waliozitumia dawa hizo? Je, kuna madhara yoyote waliyopata kutokana na kuzitumia?
Kwa kutoa taarifa sahihi, serikali itasaidia kuwatoa mashaka wanaotumia ARVs na kuwajengea imani waendelee kuzitumia bila kuathiri afya zao. Sikika inaamini kuwa kuwepo kwa dawa zenye ubora na uhakika kutaongeza imani kwa WAVIU kuendelea kuzitumia na kuimarika afya zao.
Makala hii ya Sikika imeandikwa na Aisha Hamis, Afisa Tumesikitishwa kupata taarifa kwamba watu 5,358 wanaoishi na Virusi vya UKIMWI (VVU) waliokuwa kwenye matibabu wameacha kutumia dawa za kupunguza makali ya ugonjwa huo (ARVs), mkoani Dodoma.
Taarifa kupitia vyombo vya habari na taasisi mbalimbali kuhusu Watu wanaoishi na Virusi vya UKIMWI (WAVIU) kuacha kutumia dawa, zimekuja kipindi ambacho wananchi na wadau wa UKIMWI wakitafakari hatma ya uchunguzi wa sakata la kutengenezwa dawa bandia za ARVs. Dawa hizo aina ya TT-VIR toleo namba (batch number oc.01.85) zilisambazwa katika mikoa ya Mara, Tanga na Dar es Salaam tangu Mei, 2011.
Kuwepo kwa ARVs bandia na taarifa juu ya WAVIU kuacha kutumia dawa kunadhihirisha udhaifu uliopo ndani ya mifumo na mamlaka za serikali zilizopewa kusimamia ubora, uwepo na upatikanaji wa dawa. Sikika inaamini, pengine kuna uhusiano wa karibu kati ya uwepo wa dawa hizo bandia nchini na WAVIU hao kuingiwa hofu na kuacha kutumia dawa.
Tunaamini hayo kwa kuzingatia ukweli kwamba suala la mgonjwa kutumia dawa kwa kiasi kikubwa linategemea imani na utayari wa mhusika. Uwepo wa dawa bandia ama zisizo na ubora unapunguza imani na hivyo kuweza kusababisha mgonjwa kuacha kuzitumia na kupelekea kuathirika zaidi.
Sakata la kuwepo kwa ARVs bandia lililochukua takribani miezi nane sasa, limekuwa na sura tofauti hususan juu ya nani anahusika moja kwa moja baada ya kiwanda kinachodaiwa kutengeneza dawa hizo Tanzania Pharmaceticals Industry (TPI) kukanusha kuhusika na utengenezaji huku Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) na Bohari Kuu ya Dawa (MSD) wakisisitiza kuwa dawa hizo zimetoka kiwandani hapo.
Sikika inathamini na kutambua juhudi za serikali za kutekeleza taratibu za kisheria ikiwemo ukaguzi na uchunguzi wa kimaabara uliofanywa na Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii kupitia TFDA. Hatua nyingine iliyochukuliwa na serikali ni kukifungia kiwanda cha TPI kutokana na nyaraka zilizokutwa MSD kuonesha kuwa TPI iliiuzia MSD dawa hizo. Serikali pia iliwasimamisha kazi watendaji watatu wa MSD.
Usambazaji na matumizi ya dawa aina ya TT –VIR 30 toleo namba 0C .01.85 pia ulipigwa marufuku na serikali ilizitaka mamlaka za serikali za mitaa kupitia waganga wakuu, kukusanya dawa hizo bandia kutoka vituo vya huduma za afya na kwa wananchi, na kisha kuzirudisha MSD.
Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa na MSD, takribani makopo 8,000 ya toleo hilo kati ya zaidi makopo 12,000 yaliyosambazwa yalikusanywa. Hivyo kwa hesabu rahisi, kuna takribani makopo 4,000 ambayo bado yapo kwenye mzunguko na ambayo hakuna taasisi yenye uhakika wa yalipo makopo hayo; kwenye vituo vya huduma ama kwa wananchi.
Serikali ililifikisha suala la ARVs bandia kwa Mkurugenzi wa Makosa ya Jinai (DPP) kwa uchunguzi na hatua zaidi za kisheria. Lakini, pamoja na juhudi hizo za serikali, Sikika hairidhishwi na kasi ndogo ya ufuatiliaji wa tatizo hilo hususan muda mrefu unaotumika kupeleleza.
Kwa mujibu wa taarifa kutoka ofisi ya DPP, jalada la kesi ya ARVs bandia limepokelewa na linashughulikiwa ili kupata muelekeo wa nani ahusishwe na kwa kosa gani kabla ya kuachia mamlaka husika jukumu la uchunguzi wa kina. Kwa maelezo ya ofisi hiyo, suala la ARVs bandia limechukua muda mrefu (zaidi ya miezi miwili), tofauti na muda wa kawaida wa siku 14 unaotumiwa na ofisi ya DPP kushughulikia kesi mbalimbali zinazofikishwa hapo, kutokana na uzito/unyeti wa suala hilo.
Wakati taratibu hizo za kitaalamu na kisheria zikiendelea, tunaishauri serikali kutoa taarifa rasmi kwa wananchi juu ya dawa bandia (makopo 4,000) ambazo hazijakusanywa. Je, ziko vituoni au zilishatumiwa na wananachi? Kama zilishatumiwa, je serikali ina taarifa zozote juu ya waliozitumia dawa hizo? Je, kuna madhara yoyote waliyopata kutokana na kuzitumia?
Kwa kutoa taarifa sahihi, serikali itasaidia kuwatoa mashaka wanaotumia ARVs na kuwajengea imani waendelee kuzitumia bila kuathiri afya zao. Sikika inaamini kuwa kuwepo kwa dawa zenye ubora na uhakika kutaongeza imani kwa WAVIU kuendelea kuzitumia na kuimarika afya zao.
Makala hii ya Sikika imeandikwa na Aisha Hamis, Afisa Programu