Mama

Nani kama Mama .

Afya ya Mimba

Mwanamke anayetaka kubeba mimba anashauriwa aache kunywa pombe na kuvuta sigara.

Mama na Mtoto

Mazingira mazuri ya Afya ni Moja ya njia ya kuepuka matatizo ya mama wakati wa kujifungua.

Tuwalinde watoto

watoto 200 kati ya 100,000 wanapoteza maisha wakati wa kuzaliwa na baada ya kuzaliwa, idadi hii ya vifo ni kubwa sana hapa nchini Tanzania.

Karibu kwenye blog hii kwa Habari za Afya ya Mama na Mtoto.

Kufikia mwaka 2010, takwimu zilikuwa zinaonesha kwamba kila wanawake 454 katika vizazi hai 100,000 walikuwa wanapoteza maisha wakati wa ujauzito au kujifungua kwa matatizo mbalimbali ya uzazi.

watoto 200 kati ya 100,000 wanapoteza maisha wakati wa kuzaliwa na baada ya kuzaliwa, idadi hii ya vifo ni kubwa sana hapa nchini Tanzania..

Thursday, March 28, 2013

KUKOSEKANA KWA ARV KWACHANGIA WATOTO KUZALIWA NA VVU

Zarula Rajabu (30) anaishi na virusi vya ukimwi,anawatoto wanne kati ya hao mtoto mmoja ana maambukizi ya virusi vya ukimwi, anishi katika kijiji cha Matekwe katika kata ya Kilimarondo wilaya ya Nachingwea mkoa wa Lindi. Zarula aligundulika na vvu akiwa na ujauzito wa miezi sita, alipohudhuria kliniki ya zahanati ya Matekwe kwa mara ya kwanza. Lakini hakupewa dawa za ARVs za kumkinga mtoto aliyetumboni asipate na maambukizi ya virusi vya ukimwi. “Ningepatiwa...

Sunday, March 24, 2013

GOFU LA NYANZA CO-OPERATIVE UNION

Gofu la chama cha ushirika cha Nyanza lililopo katika kijiji cha Nassa katika wilaya ya Nyashimo mkoa mpya wa Simiyu. Ndani ya gofu hilo kuna vinu vya kuchambua pamba na kukamua mafuta ya mbegu za pamba, kwa muda mrefu sasa vinu hivyo havitumiki na wakulima wanapeleka pamba kuchambua katika wilaya ya Bunda mkoa wa Mara. Kwa sasa wakulima wa pamba wako katika kilimo, kilo moja ya pamba kwa mwaka jana ilikuwa shilingi 630....

Thursday, March 21, 2013

KARUNGUYEYE, MUUGUZI ASIYE NA TAALUMA YA AFYA ANAYETOA HUDUMA KWA MIAKA 22

Benjamin  Karunguyeye  (55)  amefanya kazi ya kuwahudumia wagonjwa mbalimbali katika kijiji cha Ifinga, Songea kwa takriban miaka 22 sasa, pasipo kusoma katika darasa lolote la uuguzi au udaktari. Anapima na kuwazalisha wajawazito na kuhudumia watoto wa chini ya umri wa miaka mitano kwa kuwapa chanjo.  Kwa kipindi cha mwaka mmoja, kuanzia Agosti mwaka 2011 mpaka Agosti 2012, alikuwa akisimamia na kuendesha huduma zote...

Monday, March 18, 2013

UKOSEFU WA MAJI SAFI BUNDA WAPELEKEA WANANCHI KUTUMIA MAJI MACHAFU YA MITARO

  Wakazi wa wilaya ya Bunda  mkoa wa Mara, wapo hatarini kupata magonjwa ya mlipuko katika kipindi hiki cha mvua, yanayosababisha na ukosefu wa maji safi na salama. Tatizo la ukosefu wa maji safi na salama katika wilaya hiyo, ni la zaidi ya miaka 20 wakazi hao wanatumia maji ya katika marambo yanayopatikana baada ya kunyesha mvua na maji katika mifereji ya maji machafu. Mwenyekiti...

Thursday, March 14, 2013

SABABU ZINAZOWAKIMBIZA WAJAWAZITO 'LEBA' BUNDA HIZI HAPA

   Sababu kubwa inayopelekea wajawazito kujifungulia kwa mkunga wa jadi pamoja na nyumbani, ni lugha chafu za manesi, ukosefu wa vifaa tiba na madawa muhimu kwa mjamzito baada ya kujifungua. Asilimia 100 ya wajawazito wanaohudhulia kliniki kipindi cha ujauzito katika wilaya ya Bunda mkoa wa Mara, lakini 68 pekee ndio wanaorudi kujifungulia katika zahanti, kituo cha afya na hospitali, asilimia 32 wanajifungua kwa mkunga...

Wednesday, March 13, 2013

"HAKUNA ANAYEJALI VIFO VYA WAJAWAZITO NA WATOTO WACHANGA!"

HAKUNA anayejali kama mjamzito iwe kijijini au mjini anapotaabika na mimba yake wakati mtoto anayezaliwa ni mali ya taifa. Hakuna mtaalam wa afya anayejali kuona mjamzito anateseka na kushindwa kusukuma mtoto wakati wa kujifungua na hakuna anayejali kuona watoto wachanga hasa vijijini wanapokufa baada ya kuzaliwa. Hakuna anayejali kuona wanawazito kukokotwa kwenye mikokoteni ya punda na baiskeli kufuata huduma ya kujifungua. Hakuna anayejali wakunga wa jadi wanaosaidia wajawazito kujifungua salama na hakuna anayejali...

Monday, March 11, 2013

BUNDA: WATOTO 'NJITI' HATARINI KUPOTEZA MAISHA KWA KUKOSA UMEME

   Watoto wanaozaliwa chini ya miezi tisa (Njiti) wapo hatarini kupoteza maisha kwa sababu ya kukosa joto la uhakika katika hospitali teule ya Bunda. Tatizo la kukosekana kwa joto katika chumba maalumu cha kuwapatia joto kwenye hospitali hiyo linasababishwa na kukatika kwa umeme mara kwa mara na kuwepo kwa mita ya luku katika hospitalini hiyo. Revocatus Kato ni Muuguzi Mkuu katika hospitali teule...

Tuesday, March 5, 2013

MASIKINI MGANGA MKUU HANA CHOO

Chooo cha waganga katika kituo cha afya cha Ikizu wilaya ya Bunda mkoa wa Mara kimetitia chini ya aridhi, choo hiki kilikuwa kinatumika na nyumba mbili za waganga katika kituo hicho, kwa sasa inawalazimu familia hizo kutumia choo kimoja na wagonjwa wanaofika kutibiwa katika kituo hicho ambacho kipo zaidi ya mita 150, hali hiyo inaweza kusababisha magonjwa mbalimbali ya kuambukiza. Ni zaidi ya miezi mitano sasa toka choo hicho kititie...

KIKWETE UNALIONA HILI!

Dk. Abahehe Kanora mganga mkuu wa kituo cha afya cha Ikizu katika wilaya ya Bunda mkoa wa Mara, akionesha Bajaji ya Kikwete ikiwa imetolewa kitanda cha kubeba mjamzito, kutokana na kushindwa kukitumia kwa ubovu wa barabara. Wilaya ya Bunda ina kata 28 kati ya hizo kata 4 tu ndio zina vituo vya afya kama Ikizu, Manyamanya na Kasuguti vituo hivyo vina Bajaji ya Kikwete lakini hazitumiki kwa ubovu wa barabara, baada ya kutoa kitanda hicho wanatumia...

Monday, March 4, 2013

HII NDIO BENDERA YA TAIFA

Bendera ya Taifa ikiwa imechanika katika wilaya ya Bunda mkoa wa Mara, Jimboni kwa Wasi...

Sunday, March 3, 2013

MALARIA INAVOMALIZA WATOTO BUNDA

Mwajuma Ramadhani mtoto wa miaka miwili na mwezi mmoja akiwa katika hali mbaya kwa kuumwa ugonjwa Malaria, Winifrida Chales mama wa Mwajuma akiwa amemkamata huku Dokta Msimu Michel akijitahidi kumpima mtoto huyo katika kituo cha afya cha Manyamanyama wilaya ya Bunda mkoa wa Mara,Ugonjwa wa Malaria ni tishio kwa watoto mbalimbali katika wilaya hiyo, asilimia 42 ya watoto wote wanaofikishwa katika zahanati, kituo cha afya na hospitali katika...