Mama

Nani kama Mama .

Afya ya Mimba

Mwanamke anayetaka kubeba mimba anashauriwa aache kunywa pombe na kuvuta sigara.

Mama na Mtoto

Mazingira mazuri ya Afya ni Moja ya njia ya kuepuka matatizo ya mama wakati wa kujifungua.

Tuwalinde watoto

watoto 200 kati ya 100,000 wanapoteza maisha wakati wa kuzaliwa na baada ya kuzaliwa, idadi hii ya vifo ni kubwa sana hapa nchini Tanzania.

Karibu kwenye blog hii kwa Habari za Afya ya Mama na Mtoto.

Kufikia mwaka 2010, takwimu zilikuwa zinaonesha kwamba kila wanawake 454 katika vizazi hai 100,000 walikuwa wanapoteza maisha wakati wa ujauzito au kujifungua kwa matatizo mbalimbali ya uzazi.

watoto 200 kati ya 100,000 wanapoteza maisha wakati wa kuzaliwa na baada ya kuzaliwa, idadi hii ya vifo ni kubwa sana hapa nchini Tanzania..

Thursday, March 28, 2013

KUKOSEKANA KWA ARV KWACHANGIA WATOTO KUZALIWA NA VVU

Zarula Rajabu (30) anaishi na virusi vya ukimwi,anawatoto wanne kati ya hao mtoto mmoja ana maambukizi ya virusi vya ukimwi, anishi katika kijiji cha Matekwe katika kata ya Kilimarondo wilaya ya Nachingwea mkoa wa Lindi.

Zarula aligundulika na vvu akiwa na ujauzito wa miezi sita, alipohudhuria kliniki ya zahanati ya Matekwe kwa mara ya kwanza. Lakini hakupewa dawa za ARVs za kumkinga mtoto aliyetumboni asipate na maambukizi ya virusi vya ukimwi.

“Ningepatiwa dawa za ARVs kipindi cha ujauzito wangu, na wakati wa kuumwa uchungu, ningemzaa mtoto wangu bila ya kupata maambukizi ya virusi vya ukimwi na angeishi maisha marefu,”alisema Zarula.

Muuguzi katika zahanati ya Matekwe Lidia Urio (51) alisema kuwa, Zarula alipohudhulia mara ya kwanza kliniki alimpima na kugundua kuwa ana maambukizi ya virusi vya ukimwi.

 “Nilimpompima na kugundua kuwa ana virusi vya ukimwi nilitakiwa kumuanzishia dawa za kupunguza makali ya ugonjwa huo, pamoja na kumkinga mtoto aliyetumboni asipate maambukizi ya virusi vya ukimwi, lakini kutona na kuharibika kwa dawa nimeshindwa kumuanzishia hiyo dozi,”alisema Muuguzi Urio.

 Aliendelea kuhudhuria kliniki mpaka muda wa kujifungua ulipofika, alijifungulia katika Zahanati ya Matekwe, lakini hata alipokuwa anaumwa uchungu hakupata dawa za ARVs ambazo zinamkinga mtoto asipate maambukizi wakati wa kuzaliwa. Ndio chanzo cha yeye kumuambukiza mtoto wake wan ne mwenye miezi saba virusi vya ukimwi.

Baada ya miezi mitatu kupita toka amejifungua, Zarula alilazimishwa kumpeleka mtoto wake ktika hospitali ya wilaya ya Nachingwea, ili atolewe damu na kupimwa kama mtoto amepata maambukizi au hajapata.

Zarula alikwenda alifanikiwa kupata pesa ya kwenda hospitali ya wilaya kumpima mtoto wake, utaratibu wa kupima watoto wa chini ya miezi 18 ni lazima mtoto anatolewa damu katika kisigino cha mguu kwa sababu umri aliokuwa nao ukimpima kwa kumtoa damu kama unavyowapima watoto wenye miezi 18 na watu wazima, huwezi kugundua kuwa anamaambukiz kwa sababu bado kuna antibody za mama mwili kwa mtoto wa chini ya miezi 18 na hapo mtoto anatakiwa kupimwa antijen zake au DNA.

Aidha damu hiyo ikipatikana inahifadhiwa kwa utaratibu maalumu, kisha kusafirishwa kwenda katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili kwa vipimo vya hali ya juu , ili kugundua kama mtoto wa chini ya miezi 18 amepata maambukizi au hajapata.

Mashine maalumu za kupima maambukizi ya virusi vya ukimwi kwa watoto wa chini ya miezi 18 hapa nchini, ziko katika kanda nne nazo ni Muhimbili Dar es salaam, Bugando Mwanza, Kcmc Moshi na Mbeya.

Katika mkoa wa Lindi na Mtwara hawana mashine hizo, inabidi damu zote za watoto waliozaliwa na mama wenye maambukizi ya virusi vya ukimwi, inawalazimu kupeleka damu zao katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili, ni gharama kubwa sana na kila baada ya wiki mbili au tatu wanapeleka damu za watoto hao.

Zarula anaficha kuwaeleza familia yake kwamba anaishi na virusi vya ukimwi, kwa sababu anahofia kutengwa kama alivyotengwa mjomba yake baada ya kusema anaishi na virusi vya ukimwi.

“Naogopa kuwaeleza ndugu zangu kwamba ninaishi na virusi vya ukimwa, wanajaziba sana; wanaweza kunitenga katika familia kama walivyomtenga mjomba, ni mume wangu pekee ndio anafahamu afya yangu kwa sasa,” alisema Zarula.

Mume wake Zarula, hajapima maambukizi ya virusi vya ukimwi toka mwezi Julai mwaka 2011, mkewe akiwa na ujauzito wa miezi sita mpaka sasa mtoto anamiezi saba, mkewe amemshauri kwenda kupima lakini amekataa.

“Mume wangu alikata kupima maambukizi ya virusi vya ukimwi, muuguzi Lidia amejitahidi kumshawishi kupima na kumueleza umuhimu wa kupima maambukizi ya vieusi vya ukimwi lakini amekataa mpaka sasa,” alisema Zarula.

Kwa mujibu wa muuguzi wa zahanati ya Matekwe Lidia alisema kuwa, umuhimu wa kupima maambukizi ya virusi vya ukimwi ni kujua kama umeambukizwa au bado, na kama umeambukizwa utapimwa kujua kinga zako za mwili zipo kwa kiasi gani, kama zimeshuka utaanzishiwa dawa za ARVs, pia ukijua kama unamaambukizi utachukua tahadhari kuwaambukiza wengine ambao hawana maambukizi ya virusi vya ukimwi.

Athumani ni mzaliwa wa mkoa wa Tanga, lakini kwa sasa anaishi katika kijiji cha Matekwe, anafanyakazi ya uchimbaji madini ya dhahabu na rubi katika machimbo ya mbwemkuru.Katika kipindi cha ujauzito wake, Zarula hakuweza kwenda katika kituo cha afya kilimarondo, kupatiwa dawa za ARVs, kwani nauli ya kwenda huko kutoka Matekwe kwa pikipiki ni zaidi ya shilingi 20,000. Ni zaidi ya kilometa 28, na hakuna usafiri mwengine. Pia hana uhakika kama akienda kituo cha afya cha kilimarondo atafanikiwa kupatiwa ARVs.

Kijiji cha Matekwe kina wakazi 2,548  kati ya hao wajawazito kwa mwaka 2012 walikuwa  84, waliojifungua 33, kati ya hao wenye maambukizi ya virusi vya ukimwi (VVU)  watatu.

Muuguzi wa Zahanati ya Matekwe Lidia, alikili kuwepo kwa tatizo hilo kwa akinamama hao waliogundulika na maambukizi ya ukimwi (VVU), kushindwa kupewa dawa za ARVs ndio imechangia kuwaambukiza watoto wakati wa kuzaliwa.

Watoto watatu walizaliwa na mama hao, ambao hawakupata dawa za ARVs walivyokuwa wajawazito, watoto wao wote watatu wamepata maambukizi ya virusi vya ukimwi.

Ulio alisema kuwa toka mwezi Juni 2011kulikuwa hakuna dawa za ARVs katika zahanati ya Matekwe, mpaka Desemba 2011, ndio dawa hizo zililetwa, muda huo wajawazito watatu walikuwa wameshajifungua na watoto walipata maambukizi ya virusi vya ukimwi.

"Dawa nilizonazo za kumkinga mtoto na maambukizi akiwa tumboni kwa mama zilikuwa zimekwisha matumizi yake, sikuweza kuwapatia dawa hizo, zingeweza kumletea madhara yeye na mtoto aliyetumboni, ulipofika muda wa kujifungua basi nikawazalisha hivyo hivyo”alisema Uliyo.

Ulio alitoa ushauri kwa wajawazito hao kwenda katika kituo cha afya kilimarondo kupatiwa dawa za ARVs, lakini walisema hawana pesa ya kukodi pikipiki mpaka katika kituo cha afya.

Zubeda Abasi (23), ni mkazi wa kijiji cha Matekwe, anaishi na virusi vya ukimwi, naye pia ana mtoto wa miezi tisa kwa sasa, alipokuwa mjamzito alihudhulia katika zahanati ya Matekwe lakini, kwa sababu dawa zilikuwa zimekiwsha muda wake katika zahanati hiyo,hakupewa dawa za ARVs, ndio chanzo cha mkumzaa mtoto wake akiwa ameambukizwa virusi vya ukimwi.

"Nilipokuwa na ujauzito wa miezi mitano, nilikwenda kliniki kupima nikaambiwa ninamaambukizi ya virusi vya ukimwi, nilishauriwa kumleta bwana aliyenipa mimba kupima, alikubali alivyopimwa akagundulika hana maambukizi, alinikimbia na kuniacha pekee yangu na mimba mpaka sasa nimejifungua mtoto anamiezi saba," alisema Zubeda.

Hakuweza kwenda katika kituo cha afya cha kilimarondo, kupewa dawa za kumkinga mtoto asipate maambukizi.

Kabla ya kushika mimba, Zubeda alikuwa anafanyakazi ya kunyoa nywele za katika saloon za kiume huko kilwa, amefanya kazi hiyo kwa muda wa miezi nane, akaamua kurudi kwao matekwe.

 Zubeda aliporudi Matekwe alipata bwana mwengine, wakaanza mahusiano bila ya kupima, baada ya mwezi mmoja katika mahusiano alishika ujauzito.Baada ya miezi mitano kupita alikwenda zahanati ya matekwe kuanza kliniki, hapo ndipo alipogundulika kuwa anamaambukizi ya virusi vya ukimwi.

"Sikupewa dawa za kupunguza makali ya ugonjwa huu nikaanza kuumwa na kudhohofu mwili, na pesa sina ya kwenda kituo cha afya cha kilimarondo kuchukua dawa niliendelea kuumwa homa za mara kwa mara mpaka nimejifungua mtoto wangu ambaye naye amepata maambukizi wakati wa kuzaliwa,"alisema Zubeda.

Dk. Daniel Magesa Mkurugenzi msaidizi wa tiba kutoka Pasada alisema kuwa, mjamzito anashauriwa kwenda kliniki mapema na kupima maambukizi ya virusi vya Ukimwi, akigundulika kama anamaambukizi anaazishiwa dawa ya nevirapine ya kumkinga mtoto asipate maambukizi akiwa tumboni.

Kwa mjamzito mwenye (VVU) akiwa na kinga chini ya 350 anatakiwa kutumia dawa ya kumkinga mtoto na maambukizi ijulikanayo kama zidovudine, na anatakiwa kutumia dawa za ARVs. Lakini, kama anakinga za juu zaidi ya 350 akiumwa uchungu anapewa dawa aina ya nevirapine.

Dawa hizo zote zinasaidia kupunguza kasi ya virusi vya ukimwi kuzaliana, na kama virusi vitapunguza kasi ya kuzaliana mjamzito atakuwa na kinga ya hali ya juu zaidi na kuweza kupambana na maradhi nyemelezi pamoja na kujifungua salama na mtoto pia kutopata maambukizi ya virusi vya ukimwi.

Mganga Mkuu wa Wilaya ya Nachingwea Mkoa wa Lindi Dk. John Sijaona alisema kuwa, upatikanaji wa dawa za ARVs ni changamoto kubwa sana kutokana na bohari ya dawa kuchelewesha madawa hayo, unaweza kuagiza na ukaletewa baada ya miezi miwili hadi mitatu na unaweza ukaletewa dawa ambazo sio unazozihitaji.

"Tatizo ni bohari ya madawa kuchelewesha madawa ya magonjwa mbalimbali yakiwemo ya ukimwi, hayaji kwa muda ule ambao tumeomba, na sio kwa dawa za kupunguza makali ya ukimwi hata vitendanishi vya kupimia maambukizi ya virusi vya ukimwi, ukienda unapewa boxi tano ambazo hazitoshi kulingana na wingi wa watu wanaohitaji upimaji, pia kuletewa dawa ambazo sio ulizoomba" alisema Dk. Sijaona

Kwa mujibu wa Dk. Sijaona alisema kuwa, upatikana duni wa dawa mbalimbali zikiwemo za ARVs, unachangiwa na baadhi ya wahudumu wa afya katika zahanati mbalimbali kukosea kujaza fomu za bohari ya madawa (MSD), fomu hizo zikikosewa hata herufi moja tuu bohari ya madawa wanaiweka pembeni hawatoi dawa, hivyo basi dawa zinakuja pungufu kwa sababu hiyo.

Dk. Sijaona alisema kuwa  changamoto nyingine ni wilaya ya Nachingwea kugawanyika mara mbili, kuna kanda a na kanda b, wanaweza kupeleka dawa kanda a kumbe na kanda b nako hakuna dawa.Pia uletaji wa dawa bila ya kushirikisha watendaji wa vijiji na hospitali ya wilaya kwa msd na kulazimishwa kusaini fomu ya madawa bila ya kukagua dawa au kujua kwamba zimefika sehemu husika, hilo nalo ni tatizo sugu kwa msd kanda ya Mtwara.

Dk. Sijaona alisema kuwa mjamzito hawezi kuanza kupewa dawa za kupunguza makali ya virusi vya ukimwi mpaka apimwe, kujua kama ana maambukizi au hana akionekana na maambukizi ndio anaanzishiwa dawa hizo.

Mahitaji ya upamaji yameongezeka kwa wajawazito kuanzia mwaka 2010 walipima wajawazito 4,472. Wanaume walipima maambukizi ya virusi vya ukimwi na wake zao walikwa 1,948.

Dk. Sijaona alisema kuwa, kwa sasa wilaya ina vituo 58 vya kupima maambukizi ya virusi vya ukimwi kwa kupitia njia ya shawishi, kupitia vituo hivyo idadi kubwa ya watu wanaohitaji huduma hiyo imeongezeka kutoka 1500 kwa mwezi hadi kufikia watu 3000 hadi 4000 wanapima. Nachingwea kuna wakazi 1,95,755.

Asilimia 28 hadi 33 ya wajawazito wanaohudhulia kliniki na kupimwa nchini Afrika Kusini wanamaambuki ya virusi vya ukimwi, mwezi Agosti mwaka 2009 zaidi ya wajawazito 776 kati ya 100,000 walipoteza maisha kwa sababu ya kuwa na kinga za mwili chini ya 200 na kutotumia dawa za ARVs ipasavyo.

Kufuatia hali hiyo nchi hiyo ikaweka mkakati mahususi wa kutumia dawa za ARVs kwa wajawazito mbalimbali, pamoja na kuwaangalia kwa ukaribu jinsi gani ya kupata dawa na matumizi ya dawa hizo pamoja na chakula na wakafanikiwa kuwapatiwa dawa wajawazito 2,000 kutoka katika mradi wa (RHRU)

Pia nchini Kenya maambukizi ya virusi vya ukimwi yameshuka kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto kutoka silimia 11 hadi asilimia 4 mwezi  mei mwaka 2010, sababu kubwa ya kushuka ni kutumia vituo vya afya kuanzi 17 hadi 26 katika eneo la magharibi mwa nchi hiyo kwenye wilaya ya vijijini kama Ndhiwa. Kwa kuwahamasisha wajawazito wakifika kliniki kupima na kuwapatia dawa za ARVs ili kumkinga mtoto aliyetumboni asipate maambukizi ya virusi vya ukimwi.

Kwa mujibu wa Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Dk. Hussein Mwinyi, huduma za kuzuia maambukizi ya Virusi vya Ukimwi kutoka kwa mama kwenda mtoto, (PMTCT) zimekuwa zikitolewa nchini tangu mwaka 2000. Hadi kufikia mwezi Desemba 2011 huduma hii imetolewa bila ya malipo katika vituo 4,603 sawa na asilimia 93.

Mwaka 2011 jumla ya wajawazito 86,875 wenye maambukizi ya Virusi vya Ukimwi walipatiwa dawa za ARVs kuzuia maambukizi kwenda kwa mtoto. Hii ni sawa na asilimia 71 ya wajawazito 122,146 waliokadiriwa kuwa na maambukizi ya VVU.

Kwa mujibu wa kitabu cha bajeti cha mwaka 2012/2013, cha wizara ya afya na ustawi wa jamii, kinaeleza kuwa jumla ya shilingi 253,468,765,171.00 pesa hizi zimetengwa kwa ajili ya kununua na kusambaza dawa, vifaa tiba na vitendanishi katika zahanati, vituo vya afya na hospitali za umma. Kati ya fedha hizo shilingi 147,423,200.00 zimetolewa na Global Fund kwa ajili ya kununua na kusambaza  dawa za malaria na ukimwi nchini.

Sunday, March 24, 2013

GOFU LA NYANZA CO-OPERATIVE UNION

Gofu la chama cha ushirika cha Nyanza lililopo katika kijiji cha Nassa katika wilaya ya Nyashimo mkoa mpya wa Simiyu. Ndani ya gofu hilo kuna vinu vya kuchambua pamba na kukamua mafuta ya mbegu za pamba, kwa muda mrefu sasa vinu hivyo havitumiki na wakulima wanapeleka pamba kuchambua katika wilaya ya Bunda mkoa wa Mara. Kwa sasa wakulima wa pamba wako katika kilimo, kilo moja ya pamba kwa mwaka jana ilikuwa shilingi 630.

Thursday, March 21, 2013

KARUNGUYEYE, MUUGUZI ASIYE NA TAALUMA YA AFYA ANAYETOA HUDUMA KWA MIAKA 22

Benjamin  Karunguyeye  (55)  amefanya kazi ya kuwahudumia wagonjwa mbalimbali katika kijiji cha Ifinga, Songea kwa takriban miaka 22 sasa, pasipo kusoma katika darasa lolote la uuguzi au udaktari.

Anapima na kuwazalisha wajawazito na kuhudumia watoto wa chini ya umri wa miaka mitano kwa kuwapa chanjo.

 Kwa kipindi cha mwaka mmoja, kuanzia Agosti mwaka 2011 mpaka Agosti 2012, alikuwa akisimamia na kuendesha huduma zote katika zahanati ya Ifinga peke yake.

Alikuwa akiwapima na kuwatibu watu wenye dalili za magonjwa mbalimbali yakiwemo ya ngono kama kaswende, kisonono, maambukizi ya gono na ukimwi. Alikuwa akiwachoma sindano, kuwasafisha vidonda na kuwang’oa meno.

“Nimeanza kazi hii ya kuwahudumia wanaifinga rasmi toka mwaka 1990, katika zahanati hii ya kijijini kwetu. Kabla ya hapo nilikuwa najaribu jaribu kwa kutoa huduma ndogo kama kusafisha vidonda,”alisema Kalunguyeye.

Kalunguyeye, ambaye hana sifa zozote za kitaaluma, alianza kutoa huduma katika zahanati ya Kanisa Katoliki, ambayo inasimamiwa na Jimbo Kuu la Songea, baada ya waganga na manesi walioletwa hapo na uongozi wa Kanisa Katoliki kuondoka.


"Ndipo hapo nami nikaanza kuibia ibia kutoa huduma mbalimbali kwa wanakijiji wenzangu, kwa sababu nilikuwa nashuhudia wakifariki kwa kukosa kuhudumiwa,"alisema Kalunguyeye.

Kwa upande wake Father Roja Haule alisema kuwa, yeye amefika ifinga mwaka 2005 amemkuta Kalunguyeye akitoa huduma katika zahanati hiyo.
Kalunguyeye alianza kufanya kazi katika zahanati hii mwaka 1985. Kazi zake zilikuwa ni kufanya usafi kama kufagia, kupiga deki, kuchota maji, kusafisha vyoo na kuosha vifaa mbalimbali wanavyotumia kuoshea vidonda.

“Kipindi hicho nilikuwa anafanya usafi tu, na nikimaliza naondoka kwenda nyumbani. Lakini, ilipofika mwaka 1988, nilikuwa nabaki nikimaliza kufanya uasfi, ili kuangalia jinsi gani huduma mbalimbali zinazotolewa na  mganga na nesi, lengo langu lilikuwa kujua wananchi wanavyotibiwa ili nami niwatibu,”alisema Kalunguyeye.

Alifanikiwa kujifunza namna ya kuosha vidonda, kuchoma sindano na kutoa chanjo kwa watoto.Kalunguyeye alisema kuwa mwaka 1989 nesi na mganga waliondoka na kumuacha na zahanti bila ikiwa chini yake.

Kalunguyeye alisema kuwa kipindi hiki ambacho mganga na nesi waliondoka na kuniacha kwa muda wa miezi mitatu, ndio alianza kazi ya kutibu kama tatibu aliyesomea katika chuo cha matatibu.
Mganga na nesi waliletwa mwezi March mwaka 1989, kilikuwa kipindi cha mvua na barabara ilikuwa mbaya sana, walifika ifinga kwa shida sana, walioa huduma kwa muda wa miezi mitatu kisha wakaondoka na kuniachia zahanati peke yangu.
“Mwaka huo ndio ilikwa mara ya kwanza kuanza kazi ya kutibia watu nikiwa peke yangu, ilikuwa ngumu sana kwa sababu mambo mengi sikuwa nayafahamu, nitoa huduma ile niliyokuwa kama kuchoma sindano, kutoa dawa za malaria, kupima watoto na kupima wajawazito, ugonjwa ninaoshindwa namueleza aende kituo cha afya mabada ambako ni kilometa 87 kutoka Ifinga,”alisema Kalunguyeye.
Kazi ya kutoa huduma aliifanya kwa muda wa miezi mitatu kuanzia mwezi wa Juni hadi September, walipoletwa mganga na nesi.
Lakini, zahanati ya Ifinga ina changamoto nyingine kama  kuchelewa kupatiwa madawa pale yanapokwisha. 

“Ukienda mjini kuchukua dawa kwa Rosyita Lugongo Katibu wa afya wa Jimbo la Songea pia ndio msimamizi wa zahanati zote za Kanisa Katoriki Songea, unafikia kwenye nyumba za kulala wageni. Una weza kukaa mjini kwa wiki moja ukisubiri madawa yanunuliwe ndipo upatiwe na kurudi ifinga,gharama za kusubiri madawa unajilipia mwenyewe kwa muda wote huo, ukidai unaambiwa ofisi haina pesa, unaambulia kupewa nauli ya kurudi ifinga tu. Hicho ndio kitu kingine kinachowakimbiza waganga na manesi Ifinga. Mie nikifika mjini, nafikia kwa ndugu yangu kwa hiyo huwa sina gharama kubwa,”alisema Tobias Millinga, ambaye ni mganga wa zahanati hiyo kwa sasa.

Wakati sera ya afya ya mwaka 2007 inaeleza kuwa, serikali itashirikiana na wadau mbalimbali kuimarisha afya ya uzazi ya wanawake na wanaume, watu wenye ulemavu na wazee. Pia anaendelea kueleza kuwa serikali kwa kushirikiana na wadau mbalimbali itahakikisha utoaji wa huduma bora za afya ya uzazi katika vituo vya kutolea huduma za afya vinovyowavutia wanawake, wanaume na vijana.
Huku sera hii ikisema hivi lakini uhalisia wake haupo kabisa, kwa mfano katika zahanati ya Ifinga ambayo iliyojengwa na Kanisa Katoliki hakuna miundombinu ya maji, umeme, chombo cha darubini kinatumia mwanga wa jua, pia jengo lake ni chakavu sana na mhusika wa kujua hali halisi ya zahanati yupo lakini hawajibiki.
Rosyita Lugongo katibu wa afya Jimbo la Songea,ndiye anayesimamia utoaji wa huduma za afya na ubora wa majengo hayo ya zahanati 14 na hospitali ya peramiho zilizojengwa na Kanisa Katoliki Jimbo la Songea.
Kwa mujibu wa Father Roja Haule alisema kuwa sio ubovu wa zahanati tuu hata Kanisa la Ifinga limechoka sana, lakini Katibu wa Jimbo anaomba pesa katika mashirika ya dini huko Ujerumani lakini pesa haifanyi kazi yake inayotakiwa ya kuboresha miundombinu ya maji, umeme na kukarabati majengo.
Juhudi za kumtafuta Katibu wa Jimbo hilo, kujibu matatizo mbalimbali ya zahanati ya Ifinga, mpaka kupitia kwa Mganga Mkuu wa Hospitali ya Ruvuma Dokta. Daniel Malecela kwa kumpigia simu na kwenda kuongea ili niweze kumuhoji changamoto hizo, alikata kata kata kuona na mimi na kumwambia hataki kuongea na Mwandishi wa Habari.
Serikali inatakiwa kuwajibika katika suala la kuangalia ubora wa huduma zinazotolewa katika zahanati mbalimbali nchini, kama sera ya afya inavyosema na sio kuwaachia washikadau mbalimbali kutekeleza upatikanaji wa huduma bora.
Milinga anasema kuwa walipofika Ifinga walipokelewa na Kalunguyeye, aliwaonesha mazingira ya zahanati hiyo. Lakini alisema kuwa Kalunguyeye ni mchapakazi sana anafanya kazi ya kutoa huduma kama amesomea, kwa mfano atoa chanjo kwa watoto, anawapima wajawazito, anatoa dawa za usubi majumbani.

Tobias Milinga ndiye msimamizi wa zahanati ya Ifinga kuanzia mwezi Agosti mwaka 2012, lakini yeye anataaluma ya maabara tuu aliyosomea katika chuo cha maabara katika hospitali ya Litembo Mbinga kwa muda wa miaka miwili, na kuuza kazi ya kuchunguza magonjwa mbalimbali.
 Kutokana na uhaba wa watumishi katika zahanati hiyo ambayo ina nesi nay eye mganga wa maabara lakini anafanya kazi ya kuwaona wagonjwa na kisha kupima magonjwa yao maabara,ndio maana hata yeye alivyofika akamuachia Kalunguyeye aendelee kuzalisha wajawazito.
Kalunguyeye alisema anaipenda kazi yeka na anaifanya kwa ajili ya ndugu zake wa Ifinga, kwani walikuwa wakipata shida ya kutopata huduma za afya baada ya mganga na nesi kuondoka.
Kijiji cha Ifinga kiko mbali na kituo cha afya cha madaba ni umbali wa kilometa 87, na hospitali ya peramiho ipo umbali wa kilometa  243 kutoka katika kijiji hicho, kwa sababu hiyo mganga Milinga na Kalunguyeye ndio msaada pekee katika zahanati hiyo.

Kijijni Ifinga Kalunguyeye anafahamika kwa jina la ofisa tabibu na anajulikana hivyo kwa kazi yake ya kutoa huduma za afya kwa wanakijiji hao.

“Huduma anayotoa Kalunguyeye ni nzuri sana. Amenizalisha mtoto huyu ana miaka (22) kwa sasa unayemuona hapa, ambaye amekuwa vema mpaka nayeye ameowa na sasa nina wajukuu kutoka kwa mtoto huyu  aliyenizalisha Kalunguyeye. Nampenda sana kwa kazi ya kutoa huduma,” alisema Devota Ndunguru (40)

Kwa upande wake, Kalunguyeye anasema, “Siku ya kwanza kumzalisha mjamzito nilipata taabu kidigo. Alifika mjamzito akiwa anaumwa  uchungu na nikamwambia panda kitandani. Nikavaa gloves na kumpima kama njia ya uzazi imefunguka. Nikaona imefunguka kwa sentimita 6 hivyo nikamwambia bado. Baada ya saa mmoja kupita, nikampima tena na nikakuta njia imefunguka kwa sentimita 8. Nikamwambia sukuma. Akasukuma na mtoto akatoka vema. Baada ya hapo, kutoa kondo la nyuma ndio ilikwa  tatizo maana halikutoka haraka nami nilikuwa sijui vema kulitoa kwa mkono. Ilibidi ni mtume ndugu yake yule mjamzito akamwite mkunga wa jadi aje kulitoa na, alipofika aliingiza mkono na kulitoa nje lile kondo nami hapo ndio nikajua jinsi ya kutoa kondo,” alisema Kalunguyeye.

Kalunguyeye alisema kuwa nimejua kipimo cha sentimita ya njia ya uzazi kupitia kwa manesi mbalimbali waliofanya kazi ya kuzalisha kipindi cha nyuma.

Aidha, alisema kuwa wiki moja baada ya tukio hilo, alikuja mtoto anaumwa jino mpaka shavu limevimba kwa maumivu. Kitu cha kwanza alicho kifanya ni kumwambia mzazi wake ambane vema.
“Kisha nilamwambia ufunue mdomo wake na nikachukua kifaa cha kung’olea jino.Nikaanza kuyagonga meno yote mpaka nilipofikia katika jino bovu ndipo mtoto huyo alipiga kelele na nikajua kuwa jino hilo ndio bovu. Nikaweka ganzi kwenye bomba la sindano na kumchoma pale kwenye lile jino bovu. Baada ya nusu saa ndio nikalitoa kwa umakini ili lisivunjike.”

Changamoto kubwa anayokutana nayo katika kazi hii, ni kulipwa kiasi cha shillingi 7,000 kwa mwezi, kwani anatambulika rasi kama anafanya kazi ya usafi. Malipo yake yanatolewa na uwongozi wa Kanisa Katoliki Jimbo kuu la Ruvuma.Lakini anasema hela anayopewa haitoshi ukilinganisha na gharama za maisha zilivyo.
“Napata pesa ya kujikimu kwa kupitia kazi ninazozifanya.Kung’oa meno ni shillingi 3,000, kusafisha kidonda ni shilling 2,000 na kupasua jipu ni shilling 1,500. Napata pia hela nyingine kutokana na kutibu magonjwa mengine. Hapo ndio napata pesa ya kula na familia yangu,” alisema Kalunguyeye.

Diwani wa kata ya Ifinga Rogatusi Kianjali, alisema kuwa mwaka 2009, walikaa katika vikao vya kila mwezi vya kujadili maendeleo ya kata, na katika kikao hicho kulikuwa na wajumbe mbalimbali wa kila kata, pamoja na Father Roja Haule ambaye ni kiongozi wa Kanisa katika zahanati hiyo. Kikao hicho kiliamua kuthibitisha Kalunguyeye kuwa mhudumu wa afya wa kijiji na kumfutia majukumu ya kuchangia katika kijiji.

"Natamani kusoma kama waganga wengine juu ya taaluma hii, ambayo ninaifanya kwa muda wa miaka 22. Ningekwenda chuo cha matabibu ningeweza kufanyakazi vizuri zaidi,”alisema Kalunguyeye.

Vigezo vya kujiunga na chuo cha utabibu cha serikali hapa nchini kama Lindi, Bugando , Muhimbili na Musoma, kwa ngazi ya stashahada lazima uwe umefaulu kwa kiwango cha alama C katika masomo ya Phisikia, Bailogia na alama D kwa soma la Kemia na masomo yake ni ya muda wa miaka mitatu chuoni. Ada yake ni shilingi 600,000 na shilingi 15,0,000 kwa ajili ya mafunzo kwa vitendo. Kama mhusika hana bima, analipia shilingi 50,400  zaidi na jumla yake ni shilingi 800,400 kwa kila mwaka.

Kwa upande wa utabibu ngazi ya cheti, anatakiwa  awe amefauru somo la Bilogia na alama ya C, somo la Kemia na alama ya D na katika somo la Fizikia anatakiwa kuwa na alama D. Ada yake kwa mwaka ni shilingi 550,000 na 150, 000 ya kujifunza kwa vitendo. Pia, kama mhusika hana bima ya afya anatakiwa kutoa shilingi 50,400 na kufanya jumla ya shilingi 750,400.

Kwa upande wa vyuo binafsi kama chuo cha uuguzi cha Kanisa Katoliki ambacho kipo Ndanda, Mtwara, vigezo vinafanana na vile vya vyuo mbalimbali vya serikali ambavyo vinafundishwa utabibu, gharama kwa stashahada na cheti ni milioni 1.150,000.

Mratibu wa masomo ya kujiendeleza kwa watumishi wa afya mkoa wa Lindi, Dokta Betram Mnyani alisema kuwa kuna, umuhimu wa kijiendeleza kwa mhudumu wa afya au mfanya usafi katika seheumu za kutoa huduma. Umuhimu wake unakuja pale kunapotokea upungufu wa watumishi katika zahanati, na kulazimika huyu mhudumu kupewa kazi ya ziada ambazo yeye hajaisomea chuoni. Hii inaweza kutokea na kazi anazoweza kupewa ni kama  kugawa dawa, kumuwekea damu mgonjwa, kuchoma sindano, kusafisha vidonda, kuzalisha na kazi zingine za kitabibu wakati yeye ameajiriwa kwa kazi ya kufanya usafi katika zahanati, kituo cha afya na hospitali.

Japokuwa Kalunguyeye amekata tama ya kusoma kwa sababu elimu yake haimruhusu kuendelea mbele na,  hana uwezo wa kulipa ada ya chuo cha utabibu, anasema hana mpango wa kuacha kufanya kazi hiyo.

Pia baadhi ya wanakiji wa Ifinga wanatambua umuhimu na mchango wake.
Stella Ngonyani (27) ni mwanakijiji wa Ifinga ambaye alisema wanawake katika kijiji hicho wanamtegea sana Kalunguyeye.

Naye Mashaka Komba (32), ambaye ni mkazi wa Ifinga anaongezea kwa kusema, “tunatibiwa vizuri. Kama unaumwa homa, Kalunguyeye anakuchoma sindano. Binafsi, leo nimemleta mtoto kung’oa meno mawili, la juu na la chini. Ameng’oa asubuhi vema na jioni hii huyu mtoto anacheza kama unavyomuona.” Alisema Mashaka.

Hata hivyo, zahanati ya Ifinga inakabiliwa na changamoto mbalimbali, hususan kwenye vifaa. Mfano, haina kifaa cha kumtoa mtoto uchafu baada ya mjamzitokujifungua na haina kifaa cha kumsafisha mama ambaye mimba iliharibika. Pia, japokuwa Kalunguyeye ni msaada mkubwa kwa wanakijiji, anakosa utaalam  wa kutoa huduma hii.


Anna Ndunguru (30) ambaye ana ujazito wa miezi saba anasema Kalunguyeye ndiye anaye mpima akienda kliniki kila tarehe inapofika. Ndunguru anasema changamoto kubwa iliopo ni kukosekana au upungufu kwa vifaa.
Kuhusu huduma, Ladilaous Nyamakilau (65)  alisema, “Mzee kama mie na wanakijiji wote hapa kijijini tunamtegemea kwa huduma  nzuri ya kututibu magonjwa mbalimbali.”alisema Nyamakilau

Afisa Mtendaji wa Kijiji cha Ifinga, Zaituni Mango alisema Kalunguyeye ndiye mkombozi wa wanakijiji, kwa kuwatibu magonjwa na kuwasambazia dawa za  magonjwa ya milipuko kama surua, kuhara, usubi, tetekuanga na kipindupindu.
“Bila ya Kalunguyeye mambo yangezidi kuwa mabaya. Anafanya kazi ya kutibu wanakijiji kwa moyo mmoja na anatembea kwa saa nne hadi tano  mpaka kijiji cha pili cha Luhuji kwa mguu kutoa dawa za magonjwa ya kuambukiza na kuwapima akinamama wajawazito na watoto wa chini ya miaka mitano,” alisema Mango.

Kwa upande wake Kaimu mganga mkuu wa Wilaya ya Songea Dokta Daniel Masawe, alisema kuwepo kwa Kalunguyeye katika zahanati ya Ifinga ni kwa sababu ya uhaba wa waganga na manesi.

“Serikali kupitia Wizara husika ya afya, watuletee watumishi wa kada mbalimbali ya afya, ili kuweza kuziba pengo la ukosefu wa wakunga, manesi na waganga. Sio Ifinga tuu kwenye tatizo hili;  zahanati zetu zote zinaupungufu wa watumishi. Tunatambua mchango wake kwa wanaifinga na anawatibu lakini kwa mujibu wa sheria na taratibu za utumishi wa umma, hana vigezo vya kuajiriwa kama mhudumu wa afya. Kilichofanyika na Serikali ya kijiji cha Ifinga ni kumfutia kutoa michango ya maendeleo ya kijiji kama kutoa ushuru na kutoa tofali za ujenzi wa shule.”  

Kitabu cha ikama cha mwaka 1999 kinaeleza kuwa watumishi katika zahanti wanatakiwa kuwa watano, wa kada mbalimbali. Wanaohitajika ni afisa tabibu wawili wenye kiwango cha elimu cha stashahada ya juu ya tabibu na stashahada ya tabibu.

Kwa upande wa nesi, wanatakiwa kuwa wawili; mmoja anatakiwa na stashahada ya uuguzi na mwengine anatakiwa kuwa na cheti cha uuguzi Pia, zahanati inapaswa kuwa na mhudumu wa afya aliyependekezwa na kijiji husika, lakini kabla ya kuanza kutoa huduma, anatakiwa kupewa mafunzo ya msingi ya mwaka mmoja.

Kituo cha afya kinatakiwa kuwa na watumishi 28. Wanahitajika waganga wawili wenye elimu ya stashahada ya juu na ofisa tabibu mwenye stashahada. Nesi wanatakiwa kuwa wanne wa kada mbili tofauti, kada ya kwanza ya nesi ni ya elimu ya stashahada ya juu na kada ya pili ni ya stashahada uuguzi. Pia  anahitajika msaidizi, awepo mtaalamu wa teknologia ya maabara mmoja, na anatakiwa mgawa dawa mmoja mwnye elimu ya stashahada ya madawa. Wengine ni, afisa afya  msaidizi wenye elimu ya stashahada na msaidizi wa  afya ya mazingira mwenye elimu ya ngazi ya cheti.

Aidha, katika kituo cha afya pia kunatakiwa kuwa na wahudumu wa afya wasiopungua watano  wenye  elimu ya kidato cha nne pamoja na kusomea kozi ya mhudumu wa afya kwa mwaka mmoja, mhasibu, seketari, fundi wa umeme na vifaa mbalimbali vya hospitali, mfanya usafi na  mlinzi.

Kwa upande wa hospitali, kunatakiwa kuwa na watumishi wa kada mbalimbali wapatao 195.

Changamoto kubwa iliyopo kwa sasa katika serikali ya Tanzania  ni uhaba wa watumishi mbalimbali katika kada ya afya. Kwa sasa, daktari mmoja anahudumia wagongwa 30,000 na nesi mmoja anatibu wagonjwa 23,000. Hi ni kwa mujibu wa Rais Jakaya Kikwete, katika hutuba yake ya kila mwezi Agosti mwaka jana.

Katika hotuba hiyo, rais alisema  kuwa wanalijua tatizo hilo na wameanza kulitatua kwa kujenga vyuo mbalimbali vya madaktari kama Chuo cha Mloganzila, shule ya kufundisha madaktari pamoja na kupanua mafunzo ya manesi na wakunga

Monday, March 18, 2013

UKOSEFU WA MAJI SAFI BUNDA WAPELEKEA WANANCHI KUTUMIA MAJI MACHAFU YA MITARO

 
Wakazi wa wilaya ya Bunda  mkoa wa Mara, wapo hatarini kupata magonjwa ya mlipuko katika kipindi hiki cha mvua, yanayosababisha na ukosefu wa maji safi na salama.

Tatizo la ukosefu wa maji safi na salama katika wilaya hiyo, ni la zaidi ya miaka 20 wakazi hao wanatumia maji ya katika marambo yanayopatikana baada ya kunyesha mvua na maji katika mifereji ya maji machafu.
Maji-shida
Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Joseph Marimbe alisema kuwa, tatizo la maji kwa Bunda ni la miaka zaidi ya 20, na kusababisha wananchi wanapata magonjwa mbalimbali ya mlipuko  kwa kukosa maji safi na salama.
"Tatizo la maji lipo tena kubwa sana hapa Bunda, maana miundombinu ya maji kama mabomba yalijengwa mwaka 1970, kipindi hicho kulikuwa na wakazi wapatao 70,000 lakini kwa sasa kuna wakazi wapatao 400,000 na bado wanatumia miundombinu ileile ya maji ya miaka 70,"alisema Marimbe.
Aidha alisema kuwa kwa sasa ndio wameanza kujenga miundombinu mipya ya maji kama mabomba na mateki, mradi huo ukikamilika utagharimu shillingi Bilioni 30, unafadhiliwa na Bank ya Afrika, Bank ya Dunia na Serikali ya Tanzania.
Marimbe alisema kuwa mradi huo wa maji ukikamilika utadumu kwa zaidi ya miaka 20, kwa wakazi hao kupata maji safi na salama na kupunguza magonjwa mbalimbali ya mlipuko kama kipindupindu na kuhara, lakini yeye kama Mwenyekiti wa Halmashauri hafahamu mradi huo utakamilika mwaka gani.
Joseph-Marimbe
Joseph Marimbe, Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya Bunda akifafanua juu ya tatizo sugu la maji kwa zaidi ya miaka 20
Kwa upande wake Mganga Mkuu wa wilaya hiyo Dokta Rainer Kapinga alisema kuwa, tatizo la magonjwa ya mlipuko kwa Bunda ni kubwa kwa kutokana na kukosa maji safi na salama.

Dokta Kapinga alisema kuwa mwaka 2010 kulikuwa na kambi za kipindupindu zaidi ya saba, na wagonjwa wapatao 97 kati ya hao wagonjwa 13 walipoteza maisha kwa kuugua ugonjwa huo.

"Kwa sasa bado hatujapata tatizo la kipindupindu ila kuna tatizo sugu la ugonjwa wa Mkojo Mchafu U.T.I, Kuhara na ugonjwa wa Ngozi kwa sababu ya matumizi ya maji machafu wanayojichotea ovyo wakazi mbalimbali wa Bunda," alisema Dokta Kapinga.

Aidha alisema kuwa katika magonjwa kumi yanayoitesa wilaya hiyo, magonjwa manne yanatokana na matumizi ya maji machafu, wanayotumia wakazi wa hapa, magonjwa hayo ni Malaria, Kifua, Kichomi, Kuhara, Kipindupindu, ugonjwa wa Ngozi, U.T.I, magonjwa zinaa kama Kisonono, maambukizi ya Gono, Kaswende na UKIMWI.

Kutoka katika kata ya Guta kulikokuwa na Ziwa Victoria mpaka kufika Bunda mjini ni kilometa 15 tu, kwa nini wilaya hiyo inatatizo la maji kwa miaka zaidi ya 20, dumu la maji linauzwa kuanzia sh. 200 hadi sh. 500, wakati maji ya ziwa yapo umbali wa kilometa 15? huu ni uzembe wa watawala katika wilaya hiyo.

Thursday, March 14, 2013

SABABU ZINAZOWAKIMBIZA WAJAWAZITO 'LEBA' BUNDA HIZI HAPA

  
Sababu kubwa inayopelekea wajawazito kujifungulia kwa mkunga wa jadi pamoja na nyumbani, ni lugha chafu za manesi, ukosefu wa vifaa tiba na madawa muhimu kwa mjamzito baada ya kujifungua.

Asilimia 100 ya wajawazito wanaohudhulia kliniki kipindi cha ujauzito katika wilaya ya Bunda mkoa wa Mara, lakini 68 pekee ndio wanaorudi kujifungulia katika zahanti, kituo cha afya na hospitali, asilimia 32 wanajifungua kwa mkunga wa jadi na nyumba kwa kusaidiwa na ndugu zao.

Ni kwa nini hasa manesi na wauguzi wa Bunda wanakuwa na lugha chafu kwa wajawazito mbalimbali, kwa sababu wako wachache na watejao wao ni wengi na hawana muda wa kumpunzika na hawalipwi pesa ya ziada katika kazi wanayoifanya.

Kwa mfano nesi na muuguzi mmoja katika wilaya hiyo kwa siku anahudumia wateja 60, wateja hao wakiwemo wajawazito kwa hali hiyo nesi na muuguzi huyu hawezi kutoa huduma bora kwa wateja zake kwa kutokana na wingi wa wateja kwa siku na malipo ya ziada baada ya kazi hayaoni.

Sofaeti Majanjara ni muuguzi katika hospitali teule ya bunda anasema kuwa, kwa siku anapokea wajawazito kuanzi 15 hadi 20 wote wanataka huduma ya kujifungua na yeye yuko zamu peke yake hana mtu mwengine wa mkumsaidia.

"Huwezi amini nafanya kazi hii kwa shida sana kwa sababu natoa huduma muhimu kwa wajawazito kujifungua, lakini naingia leba peke yangu bila ya kuwa na nesi au muuguzi wa kunisaidia, muda mwengine mama anajifungua peke yake kwa sababu nashindwa kujigawa na muda mwengine unakuta wajawazito sita wote wanaumwa uchungu wanataka kujifungua muda mmoja," alisema Majanjara

Majanjara alisema kuwa sio tuu wingi wa wateja zangu lakini pia hakuna vifaa vya kutosha kuweza kumsaidia mjamzito kujifungua vema, kwa mfano grove, sindano ya (oxytocin) kwa ajili ya kusinyaa kwa mfuko wa uzazi ili mama asipoteze damu nyingi baada ya kujifungua.

Sindano nyingine ni (maginesiam salfute) hii inamsaidia mjamzito mwenye tatizo la kifafa cha uzazi, anapoanza kuumwa anatakiwa kuchomwa dawa hii ili apone na kujifungua salama, hakanu nyuZi za kumshona mama ambaye amefanyiwa upasuaji.

Vifaa hivi ni vya muhimu sana kwa mjamzito anapoingia labe lakini katika zahanati, kituo cha afya na hospitali havipo, hivyo inamlazimu mjamzito kuvinunua katika maduka ya madawa na kukwenda navyo labe wakati wa kujifungua.

Kama mjamzito hana pesa ya kununua vifaa na dawa je anawezaje kukubali kwenda kujifungua katika hospitali wakati hana kifaa chochote, ndio hiyo asilimia 32 wanakwenda kujifungulia kwa mkunga wa jadi na nyumba kwa kukosa pesa ya kununua vifaa na kukimbia matusi, kashifa na vipigo kwa manesi na wauuguzi.
Kitanda-mkunga-jadi
Kitanda cha mtoto kwa mkunga wa jadi
Wilaya ya Bunda ina watumishi wapatao 362 lakini mahitaji ni 96, lakini kuna vijiji 106 na kila kijiji kina wakunga wajadi wawili jumla wanafika wakunga wa jadi 212 katika wilaya hiyo, wakunga hao sio tuu kuzalisha kinamama bali hata lugha na tabia kwa wateja zao ni nzuri ukilinganisha na hospitali ambako kuna mtaalamu.

Bunda inawakazi wasiopungua 3,75000 lakini vifo vya wajawazito kuanzia mwaka 2007 vilikuwa 310 kwa vizazi hai 100,000 kwa mwaka jana vimeshuka mpaka kufikia 77 kwa vizazi hai 100,000, lakini je takwimu hizi ni kwa wale wanaofika kujifungua hospitali na wanaojifungua nyumbani.

Mganga Mkuu wa wilaya hiyo Dokta Rainer Kapinga anakili kwamba vifo vilivyolipotiwa kwa wajawazito ni kwa wale wanaojifungua katika zahanati, kituo cha afya na hospitali, lakini kwa ile asilimia 32 wanaojifungua kwa mkunga wa jadi na nyumbani haijui kwa sababu ya kutojifungulia katika vituo vya kutoa huduma.
Mganga-Mkuu-Bunda
Mganga Mkuu wa wilaya Bunda Dokta Rainer Kapinga akifafanua matatizo ya wajawazito Wilayani Bunda
"Idadi ya vifo itakuwa kubwa kwa sababu wanaojifungua nyumbani ni wengi sana na hakuna taalifa yoyote tunayoipata kutoka kwa watendaji wa vijiji kwa sababu mjamzito amejifungulia nyumbani au kwa mkunga kwa hiyo wengi hawatoi hiyo taalifa," alisema Dokta Kapinga.

Katika kijiji cha Kambubu nakutana na mkunga wa jadi maalufu kama mama Nyangi, yeye ameanza kazi ya ukunga wa jadi akiwa na miaka 20, kwa sasa anamiaka 62 bado anafanyakazi ya ukunga wa jadi tena ndio tegemeo kwa wajawazito katika kijiji cha kambubu  ambacho kinazidi ya wakazi 4,000.
Nyangi
Nyangi, Mkunga wa jadi akinionesha dawa ya asili inayomsaidia mjamzito kusukuma kondo la nyuma la uzazi kama limegoma kutoka
"Kazi ya ukunga nimerithi kutoka kwa mama yangu alikuwa ananifundisha kuzalisha wajawazito mbalimbali kipindi cha uhai wake, nami nimejua mpaka sasa naendelea kutoa huduma hii kwa wateja zangu mbalimbali hapa kijijini kwa malipo ya sh. 2,000 hadi 3,000, maana hii ni kazi nimepewa na Mwenyezi Mungu ya kuwazalisha wajawazito,"alisema Nyangi.

Aidha alisema kuwa mjamzito anapofika nyumbani kwake anampokea vema, anamuandalia chai ya rangi ya moto anampatia mjamzito anakunywa huku akimwangalia kwa jicho la huruma na ukaribu na kumuuliza unajisiaje kwa sasa? mtoto anataka kuja? pia anampima kwa kutumia grove za mteja na kama hana anatumia za kwake akijifungua salama anarudisha zile grove ili azitumie kwa mwengine kama amefika kwake hana.

Kabla ya kumzalisha Nyangi lazima apige goti kwa Mwenyezi Mungu aswali ili kumuomba yeye kwa kazi ile anayofanya kwa mjamzito yule, akimaliza kumzalisha namuwekea maji ya moto choo na kwenda kumuogesha kisha mjamzito anapatiwa kikombe cha uji na kurudi nyumbani kwake.

"Kondo la nyuma likigoma kutoka anamchemshia maji ya vugu vugu kikombe kimoja na kuchanganya pamoja na chimvi kisha kumpatia anywe au anatumia majani ya kiasili kumtengenezea kama juice kisha kumpatia mjamzito anywe baada ya nusu saa kondo linatoka, pia anakitanda maalumu kwa kujifungulia mjamzito na kitanda kingine kwa ajili ya kumuweka mtoto changa," alisema Nyangi

Devota Chacha ni mjamzito wa miezi sita na mkazi wa kijiji cha Kambubu, anahudhulia kliniki kama kawaida lakini hayuko tayali kwenda kujifungulia katika kituo cha afya cha Ikizu au hospitali teule ya bunda, kwa sabau ya lugha chafu za wauguzi na manesi, ghalama ya usafiri mpaka mjini pamoja na ghalama za vifaa akiingia leba.

"Nitajifungulia kwa mkunga wa jadi Nyangi kwa sababu sina uwezo wa kughalamia huduma ya kujifungua kama kituo cha afya ikizu ukiingia lazima ulipie sh. 7,500 kwa ajili ya kitanda na mchango wa mafuta ya gari wakati kituo hakina gari, mpaka unajifungua ni zaidi ya sh.20,000 hadi 30,000 wakati kwa mkunga ni sh. 2,000 hadi 3,000," alisema Devota.

Hii ndio hali halisi ya upatikanaji wa huduma kwa wajawazito mbalimbali katika wilaya ya Bunda, lakini hali bado ni tete kwa sababu kati ya wajawazito 10 basi wawili wanaupungufu wa damu kwa kukosa kula samaki wenye madini mengi, inawezekana wajawazito hawa wawili kati ya 10 wenye tatizo la upungufu wa damu ndio wanaojifungulia kwa mkunga wa jadi kama Nyangi.

Hali itakuwa mbaya zaidi kwa vifo vya wajawazito katika wilaya ya Bunda, lakini hii ni wilaya moja tuu na Tanzania ni kubwa sana na asilimia 80 ya wakazi wake wanaishi vijijini, huko nako hali ikoje ambako mimi mwandishi sijafika na kujionea kwa macho yangu.

Nani wa kuwajibika juu ya hili wananchi, wakunga wa jadi kuacha kuzalisha, viongozi wa afya upande wa wilaya au viongozi wa afya wizara? ni lini hasa Tanzania itakuwa haina vifo vya wajawazito? kila mtu anatakiwa kuangalia jukumu lake na kufanyakazi ya kuokoa wajawazito wa Tanzania kwa pamoja kwani umoja ni nguvu.

Wednesday, March 13, 2013

"HAKUNA ANAYEJALI VIFO VYA WAJAWAZITO NA WATOTO WACHANGA!"

HAKUNA anayejali kama mjamzito iwe kijijini au mjini anapotaabika na mimba yake wakati mtoto anayezaliwa ni mali ya taifa. Hakuna mtaalam wa afya anayejali kuona mjamzito anateseka na kushindwa kusukuma mtoto wakati wa kujifungua na hakuna anayejali kuona watoto wachanga hasa vijijini wanapokufa baada ya kuzaliwa.

Hakuna anayejali kuona wanawazito kukokotwa kwenye mikokoteni ya punda na baiskeli kufuata huduma ya kujifungua. Hakuna anayejali wakunga wa jadi wanaosaidia wajawazito kujifungua salama na hakuna anayejali kutimiza ahadi kuhakikisha huduma bora za afya kwa mama na mtoto chini ya miaka mitano.

Hakuna anayejali kutenga bajeti za uhakika kwa ajili maji safi vijijini. Hakuna anayejali kusogeza kwa vitendo huduma za afya katika vitongoji na hakuna anayejali kuona kupunguza mila na desturi kwamba wajawazito kujifungulia nyumbani ni ujasiri.

Hakuna anayejali kusikia wajawazito wakitolewa kauli chafu kutoka kwa baadhi ya watoa huduma za afya. Hakuna anayajali kutatua kwa dhati tatizo la uhaba wa vitendea kazi katika huduma za afya. Hakuna anayejali ukosefu wa maji safi katika vituo vya afya hospitali na zahanati.

Hakuna anayajali kutenga na kuweka sehemu ya kupumzika wajawazito kabla na baada ya kujifungua hasa kwenye zahanati. Hakuna anayejali kutoa elimu ya uzazi wa mpango kwa jinsi zote badala yake elimu hiyo inatolewa kwa upande wa wanawake ambao ‘’wanaiba’’ kutumia huduma hiyo na wakibainika na waume zao wanapigwa na wengine wamepoteza maisha.

Hakuna anayejali kuona mimba za utotoni zikiendelea kutokea kila siku kutokana na mila na desturi, hakuna anayejali sheria mbaya ya ndoa na mkanganyiko kati ya sheria ya ndoa inayoruhusu msichana wa miaka 14 kuolewa kwa idhini ya wazazi wake na katiba inayomtambua mtu mzima kuwa ni yule mwenye miaka 18.

Hakuna anayejali kuona wanaume wananyanyaswa na wake zao na kulazimika kukimbia ndoa na kuwaacha watoto wakiteseka huku wengine wakipoteza maisha na hakuna anayejali kuona watoa huduma za afya wakiishi umbali mrefu na maeneo yao ya kazi.

Inasikitisha kuona hakuna anayejali malalamiko ya wataalamu wa afya kuendelea kununua dawa za wagonjwa kwa mfumo mbovu wa MSD wakati mfumo huo ni mbovu na dawa zinazotakiwa kuuzwa kwa shilingi 10,000 zinauzwa shilingi 30,000 kupitia watendaji wa serikali wanaohusika na manunuzi.
Hakuna anayejali kuona mtumishi anaacha taaluma yake ya awali na kujiunga na masomo ya ununuzi wa umma kwasababu huko ndiko kwenye rushwa na uchafu usioandikika wa wizi wa fedha na mikataba mibovu.

Mambo kadhaa niliyoyaanisha hapo juu yapo wilayani Bunda mkoani Mara ambako kuna idadi kubwa ya vifo vya akina mama na watoto wenye umri chini ya miaka mitano vinavyotokana na uzazi nchini Tanzania.

Baadhi ya wananchi wanaopata huduma za afya katika kituo cha afya cha Ikizu kilichopo katika kijiji alichozaliwa Jaji Joseph Sinde Warioba wananungunika kuwa Rais Jakaya Kikwete ameshindwa kutekeleza ahadi yake ya kupeleka gari la wagonjwa katika kituo hicho.

Wanasema kuwa kukosa gari kwa kituo hicho cha afya kunasababisha wagonjwa wakiwemo wajawazito wanaotakiwa kufanyiwa upasuaji kukodi ‘’Toyo’’pikipiki ili kupelekwa hospitali teule ya wilaya.

‘’Tunalazimika kukodi ‘’Toyo’’ au ‘’michomoko’’ tax kwa Sh.30,000 ili kuwapeleka wagonjwa ‘’DDH’’ hospitali ya wilaya’’ walisema baadhi ya wananchi ambao waliomba hifadhi ya majina yao.
Mbali na hilo, baadhi yao wanaulalamikia uongozi wa kituo hicho cha afya cha Ikizu kuwa unawauzia damu ya kuongezea wagonjwa kati ya Sh.15,000 mpaka Sh. 20,000 kwa unit moja(mfuko).

Mganga mkuu kiongozi wa kituo hicho cha afya cha Ikizu kilichopo eneo la kata ya Nyamuswa tarafa ya Ikizu Dr.Abahehe Kanora, anasema kuwa kituo hicho hakina gari la wagonjwa na walitegemea kuwa Rais Kikwete angewapelekea kutokana na ahadi yake alipokuwa akiomba kura kwa wananchi wa eneo hilo mwaka 2010.

‘’Hapa kulikuwa na gari Pick up lakini iliuzwa na kuharibika mwaka 1996 na wilaya ina ambulance moja tu, tegemeo letu kubwa pamoja na wananchi ilikuwa ni kutimia ahadi ya Rais Kikwete ambapo aliahidi pale njia panda kwenye mti wa kumbukumbu ya Chifu Makongoro aliposimamishwa na wananchi mwaka 2010’’ anasema Dr. Kanora.

Kuhusu usafiri kwa wajawazito wanaokwenda kujifungua katika kituo hicho, anasema wanasafiri kwa pikipiki na wanaotakiwa kufanyiwa upasuaji wanalazimika kukodi gari maarufu kwa jina la michomoko kisha kupelekwa hospitali teule ya wilaya (DDH) iliyopo umbali wa kilomita 24.

Akizungumzia uhalisia wa kituo hicho ha afya, Dr. Kanora anasema kuwa mbali na tatizo la gari la wagonjwa, pia kuna tatizo la upatikanaji wa dawa kutokana na mfumo wa manunuzi ya umma unaowalazimisha kununua dawa zote katika bohari ya serikali yaani MSD ambapo dawa hupelekewa pungufu tofauti na mahitaji.

Alipoulizwa kama wajawazito na watoto hupatiwa matibabu bure kama inavyoelekezwa na sera ya afya ya mwaka 2007 ili kupunguza vifo vya makundi hayo, alisema kuwa kwanza hakuna dawa zinazopelekwa maalumu kwa ajili ya makundi hayo lakini wajawazito hupatiwa bure huduma za kujiandikisha Kliniki, kujifungua na vipimo.
Kuhusu wagonjwa wakiwemo wajawazito kuuziwa damu kwa Sh. 15,000 mpaka 20,000. Alisema malalamiko hayo si ya kweli bali uongozi wa kituo ulikubaliana na kamati ya afya ya eneo hilo kuwa kutokana na uhaba wa vitendanashi ikiwemo vifaa na dawa za kupimia damu kila anayeongezewa damu anachangia Sh. 2000.

‘’Malalamiko hayo si kweli bali kumekuwa na tabia kwa baadhi ya wagonjwa na ndugu zao wanaohitaji damu wakiambiwa kuwa hatuna damu ndipo wanalazimika kuwatafuta watu nje ya kituo na kuja nao ili kuwatolea damu hao ndiyo wanaowauzia lakini sisi hapa anayechangia damu na anayeongezewa kila mmoja hutozwa Sh. 2000’’ alisema Dr. Kanora.

Kuhusu maji alisema kuwa mpaka sasa kuna tatizo kubwa la maji na kila mgonjwa wakiwemo wajawazito lazima aende na ndugu yake ambapo baadhi ni lazima waende na maji eneo la kituo hicho cha afya.

Mpaka waandishi wa habari wanaondoka eneo hilo la kituo cha afya, wameacha na kushuhudia familia mbili za watumishi wa kituo hicho wakiwa hawana vyoo na kulazimika kujisaidia katika choo cha wagonjwa kilichopo umbali wa mita 25 baada ya choo walichokuwa wakichangia kubomoka.
Baadhi ya wajawazito na akima mama wanaonyonyesha wanaoishi katika maeneo ya Bukama, Makongoro kata ya Nyamuswa, Nyabuzumu na kijiji cha Kambubu kata ya Nyamang’uta walisema kuwa kutokana na huduma zisizoridhisha katika kituo hicho cha afya na hospitali teule ya wilaya hiyo, wanaona ni bora kujifungulia kwa wakunga wa jadi.

‘’Mimi uzao wangu huu ni wa nane lakini nina watoto watato walio hai na wengine nilijifungulia kwa mkunga wa jadi Mama Nyangi Kisizile kwasababu hospitalini kuna matusi na fedheha nyingi na wala hatusaidiwi’’ alisema Anna Japhet(35) mkazi wa Kijiji cha Kambubu.

Utafiti nilioufanya umebaini kuwa katika kijiji hicho kuna wakunga wa jadi watatu ambapo eneo la Mugara linaongoza kwa wajawazito kujifungulia kwa wakunga wa jadi.

Takwimu zinaonesha kuwa akina mama mama 185 walijifungulia kwa wakunga wa jadi waliopata mafunzo na akina mama 71 walijifungulia kwenye zahanati ya Mugara mwaka 2009.

Ingawa wakunga wa jadi wanapuuzwa na kudharaulika na wasomi wengi lakini ukweli wa utafiti unaonesha kuwa kujifungulia kwa wakunga wa jadi hasa waliopata mafunzo kunapunguza kama si kuondoa kabisa tatizo la vifo vya akina mama wajawazito, lakini hakuna msomi anayejali kuwapa mafuzo kwa dhati wakunga wote wa jadi nchini.

Naye mjamzito Agness Baraka (23) anasema mimba aliyonayo ni ya nne lakini ana mtoto aliye hai mmoja na kwamba anahudhuria kliniki lakini bado halidhishwi na huduma za hospitalini hivyo anaona bora kujifungulia kwa mkunga wa jadi ama nyumbani kama alivyojifungua mtoto wake wa kwanza.

‘’Ukienda hospitali mfano kule DDH, wanasema kuwa mjamzito anayepaswa kusaidiwa kujifungua ni yule mwenye mimba ya kwanza lakini tuliowahi kuzaa wanatulazimisha tujifungue wenyewe bila msaada wao na kama hauna pesa unaweza kufa’’ anasema Anna.

Mkunga wa jadi Veronica John Leopard(64), alisema kuwa yeye ni mmoja wa wakunga wanaosaidia wajawazito kujifungua katika wilaya ya Bunda na hata hospitali wanamjua lakini halidhishwi na huduma zinazotolewa na kituo cha afya cha Ikizu maana kila kitu ni pesa na hivi karibuni alimpeleka mwanaye kujifungulia katika kituo hicho na kujionea huduma zisizoridhisha.

Umefika wakati kama taifa kujisahihisha kwa vitendo mfano suala la bajaji za kubeba wajawazito bila kutafuna maneno hazifai na mpaka sasa hazitumiki kwasababu hazikati kona upande wa kushoto hivyo rai yangu kwa Rais Kikwete ni kuliona hilo na kutatua kero hizo hapo juu kwa vitendo ili kujenga taifa imara lenye watu wenye afya njema kwa kuanzia katika makundi hayo yaani wajawazito na watoto chini ya miaka mitano.

Monday, March 11, 2013

BUNDA: WATOTO 'NJITI' HATARINI KUPOTEZA MAISHA KWA KUKOSA UMEME

  
Watoto wanaozaliwa chini ya miezi tisa (Njiti) wapo hatarini kupoteza maisha kwa sababu ya kukosa joto la uhakika katika hospitali teule ya Bunda.


Tatizo la kukosekana kwa joto katika chumba maalumu cha kuwapatia joto kwenye hospitali hiyo linasababishwa na kukatika kwa umeme mara kwa mara na kuwepo kwa mita ya luku katika hospitalini hiyo.

Revocatus Kato ni Muuguzi Mkuu katika hospitali teule ya Bunda alisema kuwa, kuna hatari ya kuwakosa watoto wanaozaliwa chini ya miezi tisa kwa sababu ya kutokuwa na umeme wa uhakika hapa hospitali.

"Kuna chumba maalumu cha kuongeza joto ambacho ndio kinatumika kiwakuza watoto njiti, chumba hico kinatumia kifaa maalumu cha kutoa hewa ya joto ili watoto njiti  waweze kukua vema, lakini umeme ndio changamoto kwa sababu tumefungiwa mita ya luku na TANESCO ambayo umeme wake muda mwengine unaisha saa tano usiku hospitali na kuwa kiza na chumba hicho cha njiti kinashindwa kutoa joto kwa kukosa umeme," alisema Kato

Kato alisema kuwa hospitali ina jenereta lakini matumizi ya jenereta ni ghalama kubwa sana kulitumia kipindi umeme wa luku unapoisha usiku aua kukatika, kwa siku unaweza kutumia lita 70 hadi lita 100 ya disel na lita moja inauzwa sh. 2,130 hadi 2,150 kwa siku unatakiwa kuwa na pesa zaidi ya sh.2,15000 za kununua mafuta ya kutumia katika jenereta pindi umeme unapokatika au luku ikiwa imekwisha usiku wa manane.

"Tunaiomba TANESCO kutubadilishia mita hii ya luku na kutufungia mita ya kawaida kwa sababu inachangia vifo kwa watoto njiti na wajawazito akiwa katika chumba cha upasuaji halafu luku imekwisha au umeme unakatika ghafla kuna uwezekano mkubwa wa mgonjwa huyo kupoteza maisha,"alisema Kato.

Kwa upande wake Muuguzi wa wodi ya wajawazito na vichanga hospitali hapo Peter Sungwa alisema kuwa, watoto wanaozaliwa chini ya miezi tisa ni wengi sana katika wilaya ya Bunda na wengine wanatoka katika wilaya ya Musoma Vijijini na seregeti wote wanahitaji kuhifadhiwa katika chumba hicho ili kupata joto na kukua vema.

Mwaka jana zaidi ya watoto  32 njiti wazaliwa na mwaka huu mpaka kufikia mwezi wa March zaidi ya watoto 12 njiti wamezaliwa katika hospitali hii.
mtoto-njiti
Sungwa alisema kuwa sio tuu tatizo la umeme bali kuna tatizo la uhaba wa maji katika hospitali hii, kila mgonjwa anayelazwa lazima aje na ndoo ya maji ya kuoga na kufua nguo kila siku.

"Maji nayo ni tatizo sugu katika hospitali ya Bunda tunaiomba wizara husika kutuangalia kwa jicho la huruma katika suala la upatikanaji wa maji ili iwe rahisi kuendesha shughuli mbalimbali za matibabu zinazotegemea maji,"alisema Sungwa.

Rainer Kapinga ni Mganga Mkuu wa wilaya ya Bunda alikili kuwepo kwa changamoto ya umeme na maji katika hospitali teule ya Bunda, changamoto ambayo inachangia kuzorotesha utoaji wa huduma kwa wakazi wa wilaya ya hiyo na nje ya wilaya.

"Kwa sasa tunajipanga kuandika barua kwa Tanesco kuwaomba watuondolee mita ya luku na kutuwekea mita ya kawaida ili shughuli za upasuaji na mambo mengine ya matibabu yanayo hitaji huduma ya umeme yafanyike kwa wepesi," alisema Kapinga

Wilaya ya Bunda ina wakazi wasiopungua 3,75,000 wote wanategemea kupatiwa huduma katika hospitali hiyo ambayo inatatizo la upatikanaji wa umeme na maji.

Tuesday, March 5, 2013

MASIKINI MGANGA MKUU HANA CHOO

Chooo cha waganga katika kituo cha afya cha Ikizu wilaya ya Bunda mkoa wa Mara kimetitia chini ya aridhi, choo hiki kilikuwa kinatumika na nyumba mbili za waganga katika kituo hicho, kwa sasa inawalazimu familia hizo kutumia choo kimoja na wagonjwa wanaofika kutibiwa katika kituo hicho ambacho kipo zaidi ya mita 150, hali hiyo inaweza kusababisha magonjwa mbalimbali ya kuambukiza.

Ni zaidi ya miezi mitano sasa toka choo hicho kititie aridhini na hakuna jitihada zozote za makusudi kuweza kujenga choo kingine kwa watumishi hao, kwa hali hii je watoa huduma wa kituo hiki wanaweza kufanya kazi ya kutoa huduma kiukamilifu!

KIKWETE UNALIONA HILI!

Dk. Abahehe Kanora mganga mkuu wa kituo cha afya cha Ikizu katika wilaya ya Bunda mkoa wa Mara, akionesha Bajaji ya Kikwete ikiwa imetolewa kitanda cha kubeba mjamzito, kutokana na kushindwa kukitumia kwa ubovu wa barabara.

Wilaya ya Bunda ina kata 28 kati ya hizo kata 4 tu ndio zina vituo vya afya kama Ikizu, Manyamanya na Kasuguti vituo hivyo vina Bajaji ya Kikwete lakini hazitumiki kwa ubovu wa barabara, baada ya kutoa kitanda hicho wanatumia pikipiki kwenda kuchukua dawa wilayani.

Monday, March 4, 2013

HII NDIO BENDERA YA TAIFA

Bendera ya Taifa ikiwa imechanika katika wilaya ya Bunda mkoa wa Mara, Jimboni kwa Wasira.

Sunday, March 3, 2013

MALARIA INAVOMALIZA WATOTO BUNDA

Mwajuma Ramadhani mtoto wa miaka miwili na mwezi mmoja akiwa katika hali mbaya kwa kuumwa ugonjwa Malaria, Winifrida Chales mama wa Mwajuma akiwa amemkamata huku Dokta Msimu Michel akijitahidi kumpima mtoto huyo katika kituo cha afya cha Manyamanyama wilaya ya Bunda mkoa wa Mara,Ugonjwa wa Malaria ni tishio kwa watoto mbalimbali katika wilaya hiyo, asilimia 42 ya watoto wote wanaofikishwa katika zahanati, kituo cha afya na hospitali katika wilaya hiyo wanaumwa malaria ila dawa za kutibu  ugonjwa huo mpaka sasa hazipo katika wilaya hiyo.